Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 12 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 139 2022-02-16

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza mchakato wa Wilaya ya Urambo na Kaliua kutumia line yake ya umeme ili kupunguza au kumaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Wilaya hizo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rehema Juma Migilla, Mbunge wa Ulyankulu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya za Urambo na Kaliua zinapata umeme kwa njia moja inayoanzia Kituo cha Kupooza Umeme kilichopo Tabora Mjini. Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) inatekeleza mradi wa ujenzi wa Kituo cha Kupooza Umeme katika Kijiji cha Uhuru, Wilayani Urambo, kitakachopokea umeme mkubwa (Kilovolt 132) kutoka Tabora Mjini.

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa mradi unaendelea, jengo la kupokelea Umeme (Control Building) limekamilika, upimaji wa njia ya msongo wa kilovoti 132 kutoka Tabora hadi Urambo umekamilika, uthamini wa mali za wananchi watakaopitiwa na mradi umekamilika na mikataba ya wazabuni watakaoleta vifaa vitakavyotumika kwenye ujenzi (wa njia na vifaa vya umeme) imekamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kituo hicho kitakuwa na njia za usambazaji umeme (distribution lines) zinazojitegemea kwa kila Wilaya, yaani Urambo moja na Kaliua moja na hivyo kufanya ziwe na Umeme wa Uhakika zaidi. Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba, 2022.