Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha usajili wa Taasisi ya NEMC katika Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Green Climate Fund (GCF) ili kuipatia nchi fursa za fedha za mabadiliko ya tabianchi?

Supplementary Question 1

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na yenye matumaini mazuri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile mchakato wa wenzetu hawa NEMC kujiunga na Mfuko wa Fedha wa Green Climate Fund umechukua muda mrefu kuliko ilivyotaratijiwa; na kwa kuwa sehemu ya mchakato huo ilishafanyika wakati NEMC wanajisajili katika Mfuko wa Adaptation Fund.

Je, NEMC wamejipanga vipi kuweza kuainisha vipaumbele vya miradi kwa kuzingatia maeneo ya kijiografia, Zanzibar na Tanzania Bara ili wakishapata usajili wasije tena kuchelewa kuwasilisha andiko la mradi kwenye sera hizi ambazo nchi mbalimbali zinaomba na hazijatengwa kwa ajili ya Tanzania peke yake?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili: Kwa kuwa tunaenda kupata taasisi ya pili sasa kwa upande wa Tanzania Bara ambayo imepata accreditation kwa upande wa Mfuko wa Fedha wa Green Climate Fund: Je, Ofisi ya Makamu wa Rais imejipanga vipi kuisaidia Zanzibar angalau kuweza kupata taasisi moja ambayo itapata usajili kwa ajili ya Mfuko huu wa Mabadiliko ya Tabianchi ili Wazanzibar nao wawe na direct access ya kuomba hizi fedha za mabadiliko ya tabianchi? Ahsante. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Soud maswali yake ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nichukue fursa hii nimpongeze sana Mheshimiwa Soud kwa kazi nzuri anayoifanya hasa ya kutoa elimu kwa wananchi katika masuala mazima ya uhifadhi wa mazingira. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunayo maeneo ambayo tumeshayaainisha au tunayafanya kabla hatujaanza kufanya uteuzi wa hiyo miradi. Kwanza huwa tunatembelea maeneo ambayo tunaweza tukaiibua hiyo miradi ambayo tunaweza kuiingiza huko. Kingine tunachokifanya ni kukusanya taarifa ambazo zinaweza kusaidia na baadaye tunaenda kuziandikia project proposal.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto iliyokuwepo hapo ni kwamba mara nyingi miradi hii inakuwa inasuasua. Kwa hiyo, nataka nichukue fursa hii nitoe wito kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri nchini, wajitahidi wasimamie vizuri miradi hii, kwa sababu kuna baadhi ya maeneo fedha zimepelekwa, lakini bado miradi hii inasuasua haijamalizika utekelezaji wake wakati bado kuna baadhi ya maeneo miradi hii imeshakamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuisaidia Zanzibar kupata angalau taasisi; Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira ipo wazi, kikubwa ni kwamba tunawaomba waje, tutawaelekeza, tutawafahamisha, tutawaambia namna ambavyo tunaweza tukawasaidia wakaingiza hizo taasisi. Kikubwa ni kwamba wanaweza wakaandaa pia miradi ili wakija kwetu inakuwa rahisi kuifanyia utekelezaji. Nakushukuru. (Makofi)

Name

Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha usajili wa Taasisi ya NEMC katika Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Green Climate Fund (GCF) ili kuipatia nchi fursa za fedha za mabadiliko ya tabianchi?

Supplementary Question 2

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri ambaye anahusika na Mazingira katika Kikao cha Bunge kilichopita alitoa ahadi ya kuja kutembelea Kisiwa cha Pemba ili kuona athari ya mabadiliko ya tabianchi hasa katika Kisiwa cha Mtambwe Mkuu, Kojani na Kisiwa Panza.

Je, ni lini hasa atakuja kuona athari hiyo? Ahsante.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Khalifa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya Bunge hili tukijaaliwa tutajitahidi tupange ziara kwa ajili ya kwenda Kojani na maeneo mengine ya Mtambwe Mkuu kwenda kukagua maeneo hayo. (Makofi)

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha usajili wa Taasisi ya NEMC katika Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Green Climate Fund (GCF) ili kuipatia nchi fursa za fedha za mabadiliko ya tabianchi?

Supplementary Question 3

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, mabadiliko ya tabianchi yamesababishwa sana na uharibifu wa mazingira; na mara nyingi ukipita katika milima hii ya Kitonga, Nyang’oro pamoja na kule Makombe unakuta kwamba watu wamekuwa wakichoma mkaa ovyo: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka ulinzi sasa kwenye misitu hii ili uharibifu wa mazingira usiendelee. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kiswaga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tunayo mikakati mingi tunayoipanga katika kuhakikisha kwamba tunalinda mazingira, hasa katika maeneo hayo. Moja ni kwamba tunaendelea kutoa taaluma kwa wananchi kama sehemu ya wajibu wetu kuhakikisha kwamba wananchi hawaendelei na uharibifu wa mazingira.

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine kikubwa tunachokifanya, tunayo majeshi yetu kule au walinzi wetu ambao tunashirikiana nao na vikosi vingine vya ulinzi pamoja na Jeshi la Maliasili ambao mara nyingi huwa tunajitahidi kushirikiana nao kulinda mazingira katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.