Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 12 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 137 2022-02-16

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha usajili wa Taasisi ya NEMC katika Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa Green Climate Fund (GCF) ili kuipatia nchi fursa za fedha za mabadiliko ya tabianchi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), naomba kujibu swali la Mheshimiwa Soud Mohammed Jumah, Mbunge wa wananchi wa Jimbo la Donge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Makamu wa Rais ambayo ni Ofisi kiungo ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya Mabadiliko ya Tabianchi Kitaifa ililiteua Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ili liweze kuanza mchakato wa kupata Ithibati na kuwa mratibu wa fedha za Mfuko wa GCF.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwezi Mei, 2021, NEMC iliwasilisha maombi rasmi kulingana na taratibu na baada ya GCF kujiridhisha mwezi Julai, 2021 walitoa invoice kwa ajili ya kulipa ada ya kufanyiwa Ithibati. Ada hiyo imelipwa mwezi Agosti, 2021 na hivi sasa GCF kwa barua ya tarehe 10 Januari, 2022 wameiarifu NEMC kwamba maombi yao yanafanyiwa kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kwa sasa suala hili liko GCF, naomba tuwe na subira wakati GCF wanaendelea na taratibu zao za mapitio. Aidha, nitoe wito kwa taasisi zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufuata taratibu ili ziweze kupata ithibati kwenye Mfuko huo wa Green Climate Fund. Nakushukuru. (Makofi)