Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. REUBEN N. KWAGILWA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga miundombinu ya kisasa katika mnada wa Nderema?

Supplementary Question 1

MHE. REUBEN N. KWAGILWA: Mheshimwa Naibu Spika ahsante sana, naomba niulize swali moja la nyongeza kutokana na majibu ya swali langu la msingi. Mkataba aliopewa mkandarasi ambaye yupo site sasa kuujenga mnada wa Nderema, pamoja na kwamba unajenga miundombinu ya muhimu, bado kuna miundombinu ya msingi ambayo haijaainishwa kwenye mkataba na haimo kwenye mkataba, lakini miundombinu hii ni muhimu sana kwa mnada ule. Mathalani vibanda vya kupumzikia, mahali pa kupandishia ng’ombe kwenye magari pamoja na machinjio.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali haifikirii pana umuhimu sasa wa kwenda kufanya marekebisho kwenye mkataba ule ili miundombinu hii iweze kuingizwa kwenye mkataba huu wa mkandarasi aliyepo. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Reuben Nhamanilo Kwagilwa, Mbunge wa Handeni Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tumepeleka milioni 287 na mkandarasi atajenga miundombinu ikiwemo uzio, ofisi, mazizi manne, maeneo ya kushushia mifugo, lakini pia vyoo na miundombinu mengine. Hii ni hatua ya kwanza, hatua ya pili tutakwenda ku-consider miundombinu ambayo Mheshimiwa Mbunge ameisema ili tutenge bajeti kuhakikisha mnada ule unakuwa na miundombinu yote muhimu. Nakushukuru.