Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani juu ya uchimbaji wa madini ya Helium katika Kijiji cha Nyamusi hasa ikizingatiwa kuwa Wananchi wamezuiwa kufanya shughuli yoyote katika eneo lenye Madini hayo?

Supplementary Question 1

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Mwenekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Februari 2010 Wizara ya Madini wakati ule wakati akijibu swali hili ambalo liliulizwa na Mbunge wa wakati huo Prof. Sarungi majibu ya Serkali yalikuwa haya haya kuhusiana na utafiti wa eneo lile kwa madini ya Helium, miaka 10 baadae 2021/2022 GST kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam pamoja na kupita na kufanya utafiri lakini bado hawakuwahi kufika eneo lile. Leo ni miaka 12 sasa toka tumepata majibu haya lakini madini haya yameanza kuzungumzwa toka mwaka 1952. Nilitaka nipate comitment ya Sarikali sasa, kwa sababu ni muda mrefu imekuwa ikizungumziwa juu ya kufanya utafiri kwenye ya eneo lile lakini haufanyiki kwa wakati.

Je, kipindi hiki cha mwaka huu wa bajeti kwa mujibu ya Serikali eneo hili litanyiwa utafiti ili kuondokana na haya ambayo yamekuwa yakifanyika huku nyuma na wananchi waweze kunufaika na madini ya eneo lile?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili kwenye tarafa hiyo hiyo tarafa ya Jirango Kijiji cha Upege eneo la form kuna madini pale ya dhahabu na leseni amepewa mtu wa Barec toka mwaka 1997 lakini mpaka sasa zaidi ya miaka 20 na kitu hayajaanza kuchimbwa madini yale. Nataka pia nipate commitment ya Serikali ni lini sasa madini yataanza kuchimbwa kwenye eneo lile Utegi alimaarufu kama farm ili kuongeza mapato lakini kuongeza na kutoa ajira kwa vijana ndani ya Wilaya yetu ya Rorya. Nashukuru sana.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipende kwanza kumpongeza ndugu yangu Mheshimiwa Wambura Chege kwa jinsi anavyowapambania wapiga kura wake na hususan hawa wachimbaji wa madini na jinsi anavyopigania maslahi ya rasilimali ya hii ya madini iweze kufanyiwa kazi ili nchi yetu iendelee kuneemeka kwa utajiri tulionao wa madini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la kwanza kuhusu ni lini hii gesi asilia ya Helium itaanza kuchimbwa katika eneo la jimbo lake. Napenda kumjibu Mheshimiwa Mbunge kwamba tafiti za kutafuta haya madini Helium katika nchi yetu zinaendelea katika sehemu mbali mbali kama nilivyotaja katika kujibu swali lake la msingi, na hata kwa kuongezea katika bonge la Mto Rukwa kuna utafiri mkubwa ambao pia unaendelea na ambao viashiria vimeonyesha kwamba Tanzania huenda ikawa nchi ya kwanza Dunia kwa kuwa na akiba kubwa ya madini hayo kuliko nchi zote duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa hali halisi ilivyo kwa sasa hivi tafiti zinaendelea na mara tafiti hizi zitakavyojiridhisha kwamba tumepata akiba ya kutoka katika maeneo mbali mbali juhudi za kuwapata wawekezaji wa kuchimbua madini haya ya gesi asilia ya Helium yataweza kuendelea. Kwa hiyo, nimuhakikishiue Mbunge kwamba utafiti ambao tumepangia bajeti hii inayokuja uendelee kufanywa kwa kina zaidi utatuletea majibu sahihi kwamba ni lini hayo madini yataanza kuchimbwa katika jimbo lake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la pili anapenda kufahamu kwamba madini ya dhahabu ambayo nayo yamekuwa yakiendelea kufanyiwa utafiti katika Kijiji cha Utegi katika tarafa ya Gilongo katika Jimbo lake yataanza kuchimbwa lini maana tafiti zimeendelea kwa muda mfefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumhakikishia Mheshsimiwa Mbunge kwamba katika eneo hilo maeneo yaliyogundulika kwamba kuna dhahabu ni maeneo ya shamba maalum la Serikali linaitwa farm kwa jina mashuhuri. Lakini utafiti ambao umekuwa ukiendela kwa miaka mingi sasa bado unaendelea, na mara wale watafiti watakapokuwa wamejiridhisha kwamba kuna madini pale taratibu zitafuatwa kulingana na vifungu vya 95 na 96 ya sheria yetu ya madini sura 123 ili waweze sasa kupata vibali vya kuchimba madini hayo. Ahsante sana. (Makofi)