Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 11 Energy and Minerals Wizara ya Madini 133 2022-02-15

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani juu ya uchimbaji wa madini ya Helium katika Kijiji cha Nyamusi hasa ikizingatiwa kuwa Wananchi wamezuiwa kufanya shughuli yoyote katika eneo lenye Madini hayo?

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza tangu niteuliwa kuwa naibu Waziri wa Madini kuzimama katika Bunge lako tukufu, naomba nitumie nafasi hii kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa kibali cha kusimama kibali cha kusimama mbele ya bunge lako alaasiri hii ya leo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kipekee kabisa nimshukuru Mheshimiwa Raisi wetu mpendwa mama Samia Suluhu Hassan kwa kuniamini na kunipa dhamana hii kubwa ya kulitumikia Taifa letu kupitia sekta hii ya Madini na nimuahidi kwamba nitaifanya kazi hii kwa weledi mkubwa na uaminifu wa hali ya juu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya salamu hizo naomba sasa kwa niaba ya Waziri wa Madini nipende kujibu swali la Mheshimiwa Jafari Wambura Chege (Mbunge wa Jimbo la Rorya) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa taarifa kwa Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu kuwa kwa sasa hakuna maombi ya leseni za utafutaji au uchimbaji wa madini ya Helium yaliyopokelewa kutoka katika Kijiji cha Nyamusi. Hata hivyo, katika eneo hilo kuna chanzo cha maji moto ambacho kitalaam ni kiashiria cha uwepo wa madini ya Helium kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa awali na watafiti mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania Geological Survey of Tanzania au kwa kifupi (GST) inaendelea kuhakiki vyanzo vyote vyenye viashiria vya uwepo wa madini ya Helium katika maeneo mbalimbali nchini ambapo katika Mwaka wa Fedha 2020/2021 GST kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ilifanya uhakiki kwenye mikoa ya Arusha, Manyara, Singida, Dodoma na Shinyanga.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, nipende kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa katika mwaka wa 2022/2023 GST itafanya tena utafiti zaidi katika eneo hilo. Vilevile nipende kutoa taarifa kwamba Wizara yangu haijazuia wananchi kuendelea na shughuli katika eneo hilo. Hata hivyo, nitoe wito kwa wananchi kuendelea kuliacha wazi eneo hilo ili kuepusha migogoro na usumbufu iwapo madini hayo yatagundulika kuwa yapo ya kutosha kuchimbwa na wawekezaji kupatikana, ahsante sana. (Makofi)