Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapunguza gharama za vibali vya kuanzisha biashara ya kuuza pembejeo za kilimo Vijijini ambapo TFRA, TOSCI na TPRI huchukua takribani shilingi 600,000 kabla mfanyabishara hajaingiza mtaji dukani?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa vile uzalishaji wa chakula nchini kwa sehemu kubwa unawategemea wakulima wadogo ambao kipato chao kifedha ni kidogo kuweza kumudu kununua pembejeo za kilimo kwa maana ya mbolea na mbegu; na kwa vile kwa sehemu kubwa bei ya mbolea imeongezeka sana mwaka huu kutokana na ugonjwa wa UVIKO – 19 katika nchi ambazo zinazalisha mbolea: Ni lini sasa Serikali itahakikisha kwamba nchi yetu inajitosheleza kwenye uzalishaji wa pembejeo muhimu kama mbolea? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili: Nini sasa mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba mbolea na mbegu zinapata ruzuku ili wakulima wadogo waweze kuzalisha kwa tija? Ahsante. (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mhagama, Mbunge wa Madaba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la ruzuku, nataka tu nilihakikishie tena Bunge lako Tukufu kwamba maelekezo ya Mheshimiwa Rais ni kutengeneza legal framework ambayo itatusaidia kama Serikali kutoa ruzuku kwenye pembejeo ambazo ruzuku hizo zitakwenda ku-benefit wakulima. Nataka nilihakikishie Bunge lako Tukufu, tuko kwenye hatua za mwisho ku-design Stabilization Fund ambayo itahusika na masuala ya ruzuku na pale ambapo bei za mazao zinaanguka, Serikali inaweza kufanya intervention ili kuweza kuwalinda wakulima wa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hii ni ahadi ya Serikali na sisi tutaifanya kuanzia mwaka ujao wa fedha. Kuhusu suala la kujitosheleza pembejeo za kilimo kwa maana ya mbolea na viuatilifu, sasa hivi kama nchi sisi mahitaji yetu hayazidi tani 600,000 za mbolea. Tunacho Kiwanda cha INTRACOM ambacho kimewekeza hapa Dodoma kina capacity ya tani 600,000. Wenzetu wa Wizara ya Madini wametusaidia kutoa leseni kwa ajili ya upatikanaji wa phosphate na jana walikuwa Mkoa wa Manyara kulipa fidia wananchi waliozunguka eneo hilo. Wamelipa zaidi ya shilingi bilioni moja. Kiwanda hiki kitaanza trial mwezi wa Saba kufika mwaka kesho 2023 tutakuwa tumefika 100 percent capacity ya uzalishaji wa tani 600,000. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanda cha Minjingu tumewasaidia wamepata financing zaidi ya Dola milioni 20 ili waweze ku-expand capacity yao wafike tani 120,000. Nataka niwahakikishie ni drive ya Serikali kuvisaidia viwanda vya ndani viweze kufanya mambo mawili; moja kuzalisha organo-chemical fertilizer na pili, kufanya blending ili tuweze ku-blend chemical fertilizer wenyewe ndani ya nchi kwa mahitaji yetu ya nchi na tuweze ku-export. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mbegu, sasa hivi tumeanza ku-review makampuni binafsi kuyaruhusu kuanza kuzalisha mbegu ili siku moja Tanzania tuache kuwa importer wa mbegu, tuanze kuweza ku-export mbegu kwenda nje kwa mahitaji yetu. (Makofi)