Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Capt. Abbas Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Fuoni

Primary Question

MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI aliuliza: - Je, Serikali imewekeza kiasi gani cha fedha katika ununuzi wa ndege 11 za ATCL na ni lini uwekezaji huo utarudisha fedha zilizowekezwa?

Supplementary Question 1

MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Naridhika sana na majibu ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa ununuzi au uwekezaji wa hizi ndege 11 lazima uendane sambamba na mafunzo kwa wafanyakazi wake. Sasa Je, kuna juhudi gani za makusudi za kuhakikisha kwamba Serikali inasomesha wafanyakazi hao na hasa marubani, wahandisi na ma-cabin crew ili kuhakikisha kwamba hizo ndege 11 zinakuwa na wataalam wa kutosha wa kuziendesha? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuna wafanyakazi wastaafu wengi wa ATCL wanadai stahiki zao ambazo kwa muda mrefu sana hawajalipwa. Pamoja na ukweli ya kwamba Serikali mwaka 2016 waliliridhia kuchukua deni hilo, lakini kwa bahati mbaya mpaka leo hii mwaka 2022 madeni hayo hayajalipwa. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusiana na kadhia hii? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Abbas Ali Mwinyi, kama ifuatavyo : -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitambue namna ambavyo Mheshimiwa Abbas Mwinyi kwamba yeye ni bingwa hasa kwa maana ya masuala haya ya U-pilot na ana licence aina ya ATPL. Ni kweli kwamba Serikali imewekeza sana kama ambavyo nimejibu kwenye majibu yangu ya msingi kwamba imewekeza zaidi ya trilioni 1.44 na kwa msingi huo Serikali imejipanga ipasavyo kusomesha wale wote ambao kwanza marubani, na hivi sasa kupitia chuo chetu cha NIT, Chuo cha Usafirishaji Serikali imetenga zaidi ya bilioni nne kwa ajili ya ununuzi wa ndege ambazo zitatumika kwa ajili ya mafunzo kwa ajili ya marubani kwa kuzingatia kwamba kozi hizo zilikuwa zinatolewa nje ya nchi na kwa bei kubwa zaidi. Tunategemea kwamba ifikapo mwezi Agosti na Septemba, kozi hii itaanza kutolewa na tayari Serikali imeshatoa hizi fedha zote bilioni nne. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye swali la pili ambalo amezugumzia suala la maslahi hususan kwa wastaafu, ambao walikuwa watumishi wa kampuni hii ATCL na sasa wanadai maslahi yao. Ni kweli mwaka 2016 Serikali ilitoa commitment ya kulipa madeni hayo na mwaka 2017 kupitia CAG alihakiki hayo madeni.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2021, Wizara ya Fedha kwa mujibu wa sheria pia imehakiki hayo madeni na wanadai zaidi ya bilioni nne na sasa hatua za mwisho kwa ajili ya kuwalipa wastaafu na watumishi ambao walikuwa ATCL ipo kwenye hatua za mwisho ili waweze kulipwa. Ahsante. (Makofi)

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI aliuliza: - Je, Serikali imewekeza kiasi gani cha fedha katika ununuzi wa ndege 11 za ATCL na ni lini uwekezaji huo utarudisha fedha zilizowekezwa?

Supplementary Question 2

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa hii ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza kabisa nimpongeze sana Naibu Waziri kwa namna anavyojibu maswali kwa umakini na umahiri mkubwa. Ingawaje leo ni siku yake ya kwanza, Mungu ambariki sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali, je, Serikali imejipangaje kuongeza ndege nyingine ili kuweza kukidhi ushindani wa soko la ndani ya nchi na nje ya nchi? Ahsante.

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Msongozi, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Ruvuma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye majibu ya awali kwamba Serikali imenunua ndege 11 na sasa imejipanga kununua ndege zingine tano, ambazo zitagharimu trilioni 1.7. Nimpongeza sana Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa hizi fedha na hizi ndege zitaingia ndani ya nchi mwaka 2022. Kwa hiyo tutaendelea kuboresha shirika letu la ndege nchini na ndege hizo ni ndege zile kubwa kwa maana ya moja aina ya boeing Dreamliner aina ya 787-8 ambayo ina uwezo wa kubeba abiria 262. Pia ndege zingine mbili aina ya Airbus A220-300 zenye uwezo wa kubeba abiria 181 na ndege ya mizigo yenye kuweza kubeba tani 51 pamoja na ndege aina ya Dash 8400 aina ya Bombadier ambayo ina uwezo wa kubeba abiria 76. Kwa hiyo, kutoka zile 11 za awali jumlisha tano ambazo tutanunua na Serikali tayari imesha-approve bajeti zitakuwa ndege 16 jumlisha na ndege moja iliyokuwepo awali kabda ya hizi ndege 11 zitakuwa ndege jumla 17. (Makofi)