Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantatu Mbarak Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS aliuliza: - Je, ni sababu gani iliyopelekea vituo vidogo vya Polisi Kidongo Chekundu, Jang’ombe na Beit El Ras visifunguliwe na kufanya kazi kama ilivyokusudiwa?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri na yenye kuleta matumaini. Lakini pia niwapongeze kwa kuona umuhimu wa kukifungua Kituo cha Jang’ombe kwa kuweza kuwasaidia wananchi wa eneo hili. Lakini nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na kufungwa kwa vituo hivi kwa muda mrefu vinaonekana kuchakaa, na Mheshimiwa Waziri amesema kwamba pindi tu askari watakapotoka shule Moshi vituo vile vitafunguliwa. Je, wana mpango gani wa kuvifanyia ukarabati vituo vile ambavyo vimefungwa kwa muda mrefu ili viweze kuwa na mwonekano mzuri wa kiofisi? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwantatu Mbarak Khamis, Mbunge wa Kotoka Baraza la Wawakilishi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba vituo hivi ambavyo vimefungwa muda mrefu kwa vyovyote vile haviwezi kwenda kuanza bila angalau kufanyiwa ukarabati. Nitumie nafasi hii kumuomba Kamishna wa Polisi Zanzibar aweze kufanya marekebisho ya vituo hivi kabla ya kupangiwa askari baada ya kuhitimu mafunzo yao. Nashukuru.

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS aliuliza: - Je, ni sababu gani iliyopelekea vituo vidogo vya Polisi Kidongo Chekundu, Jang’ombe na Beit El Ras visifunguliwe na kufanya kazi kama ilivyokusudiwa?

Supplementary Question 2

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona niweze kuuliza swali la nyongeza. Katika Tarafa ya Bashnet tuna vituo viwili vya polisi; Kituo cha Bashnet na Kituo cha Dareda, lakini huduma hutolewa kwa saa 12 tu. Je, Serikali haioni sasa kutokana na ongezeko kubwa la uhalifu katika maeneo yale kuanzisha huduma kwa saa 24 ili kuboresha ulinzi katika maeneo hayo? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Regina Qwaray kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua, na kama nilivyoeleza majuzi, maeneo yote ambayo yana vihatarishi vya usalama ni wajibu wa viongozi wetu wa Jeshi la Polisi ngazi ya wilaya kwa maana ya ODC na RPC ngazi ya mkoa kuona wapi tuwekeze nguvu. Na kwa kushirikiana na Mamlaka zetu za Serikali za Mitaa kama wananchi wanaona upo umuhimu wa kufungua kituo kile, tuko tayari kushirikiana nao kuona uwezekano wa kuvianzisha kudhibiti matendo ya uhalifu katika maeneo hayo. Nashukuru. (Makofi)

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS aliuliza: - Je, ni sababu gani iliyopelekea vituo vidogo vya Polisi Kidongo Chekundu, Jang’ombe na Beit El Ras visifunguliwe na kufanya kazi kama ilivyokusudiwa?

Supplementary Question 3

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wilaya ya Kilombero ni miongoni mwa wilaya kongwe sana, lakini haina Kituo cha Polisi cha Wilaya, hali inayopelekea OCD na askari wake kutumia Kituo Kidogo cha Ifakara kama Kituo cha Polisi cha Wilaya. Sasa swali langu dogo tu. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakuwa tayari kutembelea Kilombero kujionea Kituo Kidogo cha Polisi Ifakara kinavyozingirwa na mafuriko kupelekea polisi wetu kwenda kazini wakiwa wamekunja suruari na kuvua viatu ili apandishe morali ya Serikali kusaidia juhudi ya Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi na Mbunge kujenga kituo cha polisi kipya?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abubakari Asenga, Mbunge wa Kilombero, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wote nipo tayari kuungana na Mheshimiwa Mbunge kufuatilia jambo hili. Nilikwenda kutembelea gereza kule Kilombero alizungumza juu ya jambo hili, muda haukuruhusu. Hivyo, nipo tayari baada ya Bunge hili kuongozana ili tukatatue tatizo lake lililotajwa. Ahsante. (Makofi)

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS aliuliza: - Je, ni sababu gani iliyopelekea vituo vidogo vya Polisi Kidongo Chekundu, Jang’ombe na Beit El Ras visifunguliwe na kufanya kazi kama ilivyokusudiwa?

Supplementary Question 4

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Katika Jimbo la Sumve, jimbo zima hakuna Kituo cha Polisi ambacho kina sifa ya kutunza silaha. Serikali kupitia Mawaziri mbalimbali wa Mambo ya Ndani imeshaahidi kuboresha Kituo cha Polisi cha Nyambiti ili kiweze kujengewa jengo la kutunza silaha.

Je, Serikali haioni kwamba umefika wakati sasa wa kuhakikisha kwamba Jimbo la Sumve na lenyewe linakuwa na Kituo cha Polisi chenye sifa ya kuwalinda watu wa Sumve muda wote? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kasalali Mageni, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wowote Serikali ya Chama cha Mapinduzi iko tayari kuwahudumia wananchi wake kwa njia zote za kiusalama. Jimbo la Sumve ni Jimbo moja katika Wilaya ya Kwimba, kwa hiyo, matarajio yangu ni kwamba kama pana haja ya kuanzisha Kituo cha Polisi cha hadhi ya Tarafa na kikawa na majengo stahiki kinaweza kutunza silaha. Naomba kupitia Bunge lako Tukufu nimwahidi Mheshimiwa Kasalali kwamba baada ya Bunge hili katika ziara yangu Kanda ya Ziwa nipo tayari kutembelea eneo lake ili kuona namna ambavyo tunaweza tukashughulikia suala la kuimarisha usalama katika eneo lake. Ahsante. (Makofi)

Name

Amina Daud Hassan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS aliuliza: - Je, ni sababu gani iliyopelekea vituo vidogo vya Polisi Kidongo Chekundu, Jang’ombe na Beit El Ras visifunguliwe na kufanya kazi kama ilivyokusudiwa?

Supplementary Question 5

MHE. AMINA DAUD HASSAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kwa kuniona na kunipa nafasi hii. Kwa kuwa Kituo cha Polisi cha Uzing’ambwa kipo ndani ya kisiwa ambacho kimejitenga na vijiji vingine na kufungwa kwa kituo hiki kumeleta kero kubwa kwa wananchi wa eneo hili pindi wanapohitaji msaada wa Kituo cha Polisi. Je, Serikali haioni kuna haja ya dharura ya kufungua kituo hiki kwa lengo la kuwasaidia wananchi wa vijiji hivi viwili? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Amina Daudi Hassan, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyoahidi majuzi kwamba tarehe 22 na 23 nitakuwa Zanzibar pamoja na mambo mengine kukagua Vituo vya Polisi vya Chumbuni, niko tayari kuungana na Mheshimiwa Amina kuangalia kituo chake hiki ili kuona uwezekano wa kukifanyia matengenezo. Nashukuru. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS aliuliza: - Je, ni sababu gani iliyopelekea vituo vidogo vya Polisi Kidongo Chekundu, Jang’ombe na Beit El Ras visifunguliwe na kufanya kazi kama ilivyokusudiwa?

Supplementary Question 6

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wilaya ya Bunda ina majimbo matatu, Bunda Mjini, Bunda na Mwibara. Tuna kituo kimoja ambacho ni chakavu hakiendani na hadhi ya Kituo cha Wilaya. Mheshimiwa Naibu Waziri anakijua, anapita pale akienda jimboni kwaeo, nimeuliza zaidi ya mara tatu swali hili.

Lini Serikali itakifanyia ukarabati Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Bunda kiendane na hadhi ya wilaya? Nilipokuwa Mbunge nilitengeneza Ofisi ya Upelelezi. Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Bunda nakifahamu na kama zilivyo wilaya nyingi na hasa wilaya mpya kinahitaji kuimarishwa.

Sasa hivi tunaendelea na ujenzi wa Vituo vya Polisi vya ngazi ya mikoa maana tunayo baadhi ya mikoa ambayo haina Makao Makuu ya RPC; na wilaya mpya ambazo zimeanzishwa tangu mwaka 2012. Naomba kumuahidi Mheshimiwa Bulaya katika mpango wetu wa ukarabati wa vituo hivyo Bunda pia itazingatiwa. Nashukuru. (Makofi)