Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 11 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 126 2022-02-15

Name

Mwantatu Mbarak Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. MWANTATU MBARAK KHAMIS aliuliza: -

Je, ni sababu gani iliyopelekea vituo vidogo vya Polisi Kidongo Chekundu, Jang’ombe na Beit El Ras visifunguliwe na kufanya kazi kama ilivyokusudiwa?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantatu Mbarak Khamis, Mbunge wa Kuteuliwa (Baraza la Wawakilishi), kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Vituo vya Polisi vya Kidongo Chekundu kilichojengwa mwaka 1993, Jang’ombe kilichojengwa mwaka 2018, na Beit El Ras kilichojengwa mwaka 1994 ni vituo vidogo vya polisi vilivyoko Wilaya ya Mjini Magharibi. Vituo hivi vilifungwa mwaka 2019 kutokana na upungufu wa askari. Kwa sasa Kituo cha Polisi Jang’ombe kimefunguliwa na kinafanya kazi saa 24 baada ya kupangiwa askari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pindi askari walioko Shule ya Polisi Moshi watakapohitimu mafunzo ya awali, kipaumbele cha ugawaji wa polisi hao kitakuwa kwenye maeneo yenye upungufu wa askari ikiwemo Wilaya ya Mjini Magharibi ili kuwezesha vituo vilivyofungwa viweze kufunguliwa tena. Nashukuru.