Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mialo katika Forodha za Nankanga na Ilanga zilizopo ndani ya Ziwa Rukwa ili kurahisisha shughuli za Uvuvi?

Supplementary Question 1

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza. Pamoja na nia njema ya Serikali kutaka kujenga mialo kwenye Forodha ya Nankanga na Ilanga, lakini kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu ndani ya Ziwa Rukwa kati ya Hifadhi ya Uwanda Game Reserve na ile Rukwa Lukwati.

Je, Serikali mna mpango gani wa kuweka alama za kudumu zitakazowafanya wavuvi wafanye shughuli zao za uvuvi bila kubughudhiwa na askari wa wanyamapori wa Uwanda Game Reserve pamoja na wale wa Rukwa Lukwati?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili: Ziwa Rukwa ni moja kati ya maziwa ambayo yana mamba wengi hapa Tanzania na imesababisha wavuvi wengi kupoteza maisha. Nataka kujua, ili kuwalinda wavuvi wetu ndani ya Ziwa Rukwa, Serikali mmejipangaje kuleta vyombo vya uokozi ndani ya Ziwa Rukwa?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Deus Sangu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la kwanza anataka mpango wetu juu ya kuweka maboya. Hili tutashirikiana na wenzetu wa Wizara ya Maliasili na Utalii ambayo ndiyo inasimamia hizi game reserves kwa ajili ya kuweza kuona namna tunavyoweza kutekeleza jambo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, halikadhalika, lile la mamba wanaokula wavuvi; kwa kuwa mamba pia ni rasilimali na inasimamiwa na Wizara ya Maliasili na Utalii, naomba nirejee tena katika jibu la mwanzo kwamba tutashirikiana na wenzetu wa Wizara ya Maliasili na Utalii na tutafanya mkutano wa pamoja ili tuweze kutafuta suluhu ya jambo hili, ikiwemo kupata vifaa vitakavyowawezesha wavuvi hawa kuweza kuokolewa. Ahsante sana.