Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Minza Simon Mjika

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 1

MHE. MINZA S. MJIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante, napenda kushukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, majibu yenye matumaini. Lakini nina swali moja tu la nyongeza.

Je, ni lini Serikali sasa itajenga chuo cha VETA katika Wilaya ya Meatu na Wilaya ya Busega? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante, naomba sasa kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Minza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye jibu la msingi, kwamba ujenzi wa vyuo hivi unalingana sawa au unaendana sawa na upatikanaji wa bajeti na upatikanaji wa fedha. Lakini naomba nimpe tu taarifa Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako tukufu, hatuishii tu kwenye ujenzi wa vyuo hivi tunakwenda mbali zaidi kwa sababu tukishajenga ni lazima tuweze kuangania namna gani ya upatikanaji wa vifaa lakini vile vile upatikanaji wa walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa Serikali imejikita katika umaliziaji wa vyuo hivi 25 na baadae sasa tutakwenda kwenye mkakati wa kuweka bajeti kwa ajili ya kufikia Wilaya hii ya Meatu, Busega na Wilaya nyingine nchini zilizobaki kwa sababu Wilaya bado ziko nyingi, nakushukuru sana.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante sana, vyuo hivi vya VETA ni muhimu sana kwa sababu husaidia katika kukuza ujuzi lakini pia vinaubua ubunifu, na kwa kufanya hivi husaidia vijana aidha kujiajiri au kupata ajira kwa haraka zaidi, asilimia kubwa ya Wilaya za Mkoa wa Mara hazina vyuo vya VETA. Ningependa kujua ni lini Serikali itajenga vyuo vya VETA walau kwa Wilaya ya Tarime, Rorya na Bunda? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika Mkoa wa Mara anaozungumza Mheshimiwa Mbunge kwenye maeneo hayo katika Wilaya hizo alizozitaja bado hatujaweza kuzifikia, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika awamu ijayo maeneo ambayo yatapewa kipaumbele ni yale ambayo hatujayafikia hivi sasa kwa karibu.

Kwa hiyo, nimwondoe wasiwasi katika mgawo unaokuja tutahakikisha kwamba maeneo haya aliyoyataja yanapewa kipaumbele na kuanza ujenzi mara moja. (Makofi)

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 3

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wananchi na Serikali ya Kijiji ya Mwambiti iliyopo Jimbo la Meatu katika Halmashauri ya Meatu imeridhia kutoa eneo lake la ekari mia moja bila fidia kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha VETA; Je, Serikali ipo tayari kupokea hati hiyo ya kieneo ili kukabiliana na vijana wanaokosa fusa zinazotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Leah Komanya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa hatua hiyo nzuri waliyoichukua ya kutafuta eneo na tayari wameshaandaa mpaka Hati na Wizara tuko tayari kupokea hati hiyo. Kwa sababu wameshapiga hatua moja mbele kwa kupata eneo na tayari wameshatafuta Hati tunaamini katika mchakato unaokuja pindi Serikali itakapopata fedha ina maana atakuwepo kwenye mgawo wa awamu hiyo.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 4

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu mafupi. Nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Kibondo ni kati ya Wilaya kongwe nchini, Wilaya hiyo haina Chuo cha VETA. Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Kibondo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Genzabuke, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Wilaya ya Kibondo bado hatujaweza kuifikia kwenye Vyuo vyetu vya VETA, ingawa tuna Chuo kikubwa kilichojengwa Kasulu ambapo ni karibu kabisa na wenzetu wa Kibondo. Kwa sasa tunawashauri wananchi wetu wa Kibondo waweze kupata huduma hii katika chuo chetu kikubwa ambacho tumejenga katika Wilaya ya Kasulu wakati Serikali inaendelea na mchakato wake wa kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi katika eneo hili la Kibondo. Nakushukuru sana.