Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya Polisi katika maeneo ya mpakani wilaya ya Nkasi?

Supplementary Question 1

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru, nimesikiliza majibu ya Serikali.

Mheshimiwa mwenyekiti, swali langu la msingi lilijikita mpakani tukiamini kwamba Wilaya ya Nkasi inapakana na nchi ya Congo na nchi ya Burundi, Kituo cha Polisi ambacho Mheshimiwa Naibu Waziri anajibu anazungumzia Daraja C, Daraja C hilo ambalo unalizungumza katika kata 10 za mwambao unazungumzia kata tano, na hao askari kila kituo ni askari watano, hakuna pikipiki, hakuna gari, hakuna usafiri wa majini wala wa nchi kavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa maeneo hayo yamekuwa yanavamiwa mara kwa mara Serikali haioni haja kwa kuwa shida yetu sio majengo ya kituo cha polisi, tunataka vituo vya Polisi vyenye hadhi ya kupambana ikitokea uvamizi kwenye maeneo ya mpaka. Hamuoni haja sasa ya kujenga vituo hivyo kwenye maeneo ya mpakani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa katika kata 10 za mwambao ambazo ndio zimekuwa zinatumiwa na hao maadui. Kata tano zina vituo; kata tano hazina.

Je, tunaomba kujua Serikali ina mpango gani wa haraka kwa kuwasaidia ulinzi wa wale watu kwa sababu sio ulinzi wa Nkasi ni ulinzi wa nchi nzima, ni lini mtajenga vituo hivyo vya polisi kwenye kata ya Korongwe, Nkinga na kata ya Kala ambayo wanavamiwa kila wakati? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani Mbunge wa Nkasi Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa uwepo wa vituo vya Polisi hasa maeneo yaliyo katika mipaka, na sio uwepo tu wa Jeshi la Polisi lakini kupitia Wizara ya mambo ya ndani Serikali inatambua umuhimu wa kuwepo hata vyombo vyengine, ili lengo na madhumuni mipaka yetu iendelee kubakia kuwepo salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa nimwambie tu kwamba katika mipaka mingi ambayo nimeizunguka wakati ule hasa nilipokuwa nipo katika Wizara ya Mambo ya Nchi, ambao naamini na Waziri huyu ambae sasa hivi ndio Waziri wa Mambo ya Ndani alikuwepo kule aliizunguka mipaka mingi. Maeneo mengi vituo vya Polisi vipo, lakini vituo hivi vipo distance kidogo na maeneo ya mipaka. baada ya kuona kwamba kwenye ile mipaka yenyewe Polisi na vyombo vyengine wapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimawambi tu Mheshimiwa asiwe na wasiwasi, Serikali itaendelea kujenga vituo vya Polisi, ili lengo na madhumuni wananchi waweze kuishi kwa amani na uatulivu ikiwa mipakani, ikiwa ndani ya miji, ikiwa pembezoni, ikiwa popote lengo na madhumuni watanzania waishi kwa amani na utulivu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia Serikali itaendelea kuhakikisha kwamba inapeleka vitendea kazi ili lengo na madhumuni zile huduma za doria na mambo mengine yapatikane katika maeneo ya wananchi, ninakushukuru.

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya Polisi katika maeneo ya mpakani wilaya ya Nkasi?

Supplementary Question 2

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti ahsante, kwa kuwa kituo cha Polisi cha Ng’ambo ambacho kipo Wilaya ya Mjini Unguja kina tataizo kama vituo kituo cha Polisi kilichozungumzwa. Na tatizo letu hasa ni uzio. Kwa sababu kituo hicho kipo katikati ya barabara pande zote, pia kimezungukwa na mitaa hatari ya magari yanaweza yakaingia ndani yakagonga kituo, au wanyama wanaofugwa mtaani wakaingia ndani na kituo hicho kipo tokea wakati wa ukolono, hakijaongezwa uzio, ulikuwa uzio wa senyenge umezungushwa na majani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Naibu Waziri aliwahi kuzungumza kwenye baraza hili tukufu kwamba wakati wowote utawekwa uzio toka bajeti tuliyoimaliza na tunaenda kwenye bajeti mpya hali hiyo haijatengamaa. Je, uzio huo utawekwa lini ili watu wa pale wapate amani? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nakushukuru, naomba sasa kujibu swala la nyongeza la Mheshimiwa bi Fakharia Mbunge wa viti maalum kutoka Mkoa wa Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo hichi ni moja ya miongoni mwa vituo vya Polisi ambavyo nimevifanyia ziara, na moja ya miongoni mwa vitu ambavyo tayari vimeshafanyika ni tathmini kwa ajili ya ujenzi wa uzio wa kituo kile, kalini wakati huo tunafanya tathmini tunaangali namna kwa sababu kile kituo ukikitazama unakuta kwamba kila pembe kimezungukwa na barabara. Kwa hiyo, the way utakavyojenga uzio kuna hatari ukaja ukajikuta kwamba unaila ile barabara. Sasa kula chote lakini usiile barabara kwasababu unaweza ukatengeneza mazingira mengine ambayo yanaweza kusababisha ajali za barabarani ambazo hazina sababu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa nimwambie Mheshimiwa kwamba tathmini imeshafanyika na sasa tunatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa kituo kile, Mheshimiwa wewe kwa niaba ya wananchi muwe na subra kidogo mtusubirie na sisi tumo mbioni kuhakikisha kwamba uzio unajengwa katika kituo kile. Ahsante.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya Polisi katika maeneo ya mpakani wilaya ya Nkasi?

Supplementary Question 3

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya za Mkoa wa Mtwara takriban zote ziko mpakani. Je, Serikali iampango gani wa kujenga kituo cha Polisi katika Wilaya Masasi katika kata za mpakani kabisa za Mnadhira, Mchauru, Sindano na Chikoropola ambapo kwa sasa kunaonekana kuna vuguvugu za vurugu kati ya wakulima na wafugaji? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Agnes Hokororo Mbunge wa Viti maalum kutoka Mtwara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tunapitisha ile bajeti yetu ya 2021/2022 moja ya miongoni mwa mambo ambayo tunakwenda kuyafanya katika bajeti ile ni kujenga vituo vingi vya Polisi na hasa yale maeneo ambayo yanautauta kiulinzi, maeneo ya mipakani na maeneo mengine ambayo tunahisi yana sababu za zaidi asilimia moja kuwepo kwa vituo vya Polisi kwa ajili ya kulinda Maisha ya wananchi na mali zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwambie Mheshimiwa kwamba awe na subra Serikali itahakikisha kwamba inajenga vituo vya Polisi maeneo mengi lakini hasa katika maeneo ambayo wameyataja ili liengi na madhumuni wananchi waweze kuishi katika Maisha ya ulinzi na usalama zaidi, Nashukuru.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya Polisi katika maeneo ya mpakani wilaya ya Nkasi?

Supplementary Question 4

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Wilaya ya Lushoto ina tarafa 8 lakini tuna vituo 5 tu vya Polisi, lakini katika Kata ya Lukozi na Lunguza ambazo ni miji midogo na hii Lunguza ipo karibu kabisa na mpaka wa nchi jirani ya Kenya, wananchi wale wametenda maeneo na wanataka kulikabizi Jeshi la Polisi ili kwa kushirikiana nao tuweze kujenga vituo vya Polisi. Je, Waziri yuko tayari kumuagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga aje akabaini yale amaeneo na shughuli za ujenzi zianze? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rashidi Shangazi Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya miongoni mwa azma kubwa ya Serikali ni kuhakikisha kwamba wananchi wanaishi kwa amani na utulivu katika maeneo yao hasa baada ya kupata ushirikiano kutoka kwa Jeshi la Polisi na vyombo vyengine vya ulinzi na usalama, na zaidi pale wananchi wanapoamua kwamba wao wenyewe wameshajitolea wako tayari kujenga kituo cha Polisi, sisi kama Serikali kama Wizara kama Jeshi la Polisi tupo tayari kutoa ushirikiano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa nichukue fursa hii kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi nimuagize RPC Mkoa wa Tanga kwa kushirikiana na OCDs wake na baadhi ya mastafu wake, wahakikishe kwamba wanakwenda kutoa ushirikiano kwa wananchi ili lengo namadhumuni kituo hiki cha Polisi kijengwe ili wananchi waweze kupata huduma ya ulinzi na usalama. Nakushukuru.

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya Polisi katika maeneo ya mpakani wilaya ya Nkasi?

Supplementary Question 5

MHE. PROF. KITILA A. MKUMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi hii. Wananchi wa mtaa wa Mavurunza Kata ya Kimara na mtaa Kibo kata ua Ubungo, tumechangishana tumejenga vituo 2 vya Polisi lakini hatujamalizia kwa sababu nguvu zimeisha. Je, Serikali inaweza ikaahidi kuingiza katika bajeti ijayo ili vituo hivi vikamilike? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Profesa Kitila Mkumbo Mbunge wa Jimbo la Ubungo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, narejea tena azma ya Serikali ni kuhakikisha wananchi wanajengewa vituo vya Polisi ili lengo na madhumuni waweze kupata pahala pa kupeleka matatizo yao, lakini pia waweze kulindwa wao na mali zao. Nimwambie tu kwamba tupo tayari kuhakikisha kwamba tunaingiza fungu maalum kwa ajili ya ujenzi wa hicho kituo ili lengo na madhumuni wananchi wa Ubungo na maeneo ya Jirani waweze kunufauika na kituo hicho. Nakushukuru sana.