Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 10 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 113 2022-02-14

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya Polisi katika maeneo ya mpakani wilaya ya Nkasi?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo ya mpakani mwambao mwa Ziwa Tanganyika katika Wilaya ya Nkasi kuna vituo vitano vya Polisi vya daraja C, ambavyo ni kituo cha Wampembe, kituo cha Namansi, Kipili, Kilando na Kabwe. Vituo hivi vinatoa huduma kwa wananchi kwa saa 24. Pia kuna tarajiwa kujengwa kituo kingine cha Polisi cha Daraja C katika eneo la Mpasa. Vituo vyote hivyo vinakidhi mahitaji ya kutoa huduma katika eneo la mpakani kando ya ziwa Tanganyika katika Wilaya ya Nkasi. Aidha, Serikali imepanga kuimarisha huduma kwenye vituo hivyo kwa kuvipatia usafiri stahiki hatua kwa hatua kulingana na upatikanaji wa fedha. Nakushukuru.