Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: - Je, lini Serikali inafungua Ubalozi Mdogo katika Jiji la Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na nichukue nafasi hii kuipongeza Sarikali kwamba imefuata usauri wa wabunge na ushari wa kamati na pia kama Mbunge ni jambo ambalo nimekuwa nikilisema toka mwaka 2016 na hatimae Ubalozi mdogo umefunguliwa katika Jiji la Lubumbashi, kwa hivyo itarahisisha sana utendaji wa kazi na biashara kati ya nchi yetu na nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo ninaswali moja tu la nyongeza. Kwa kuwa kwa upande wa Ziwa Tanganyika upande ule wa Kalema tayari Serikali yetu imeshaanza ujenzi wa bandari na inaendelea vizuri, lakini upande wa pili ambao kuna kama mwalo wa moba ambao sio bandari hasa haujawa katika mazingira ambao yanaweza ku-facilitate meli na hivyo sisi kufanya biashara.

Je, Serikali iko tayari kukutana na Serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo kupitia tume ya pamoja na hivyo kushirikiana na kuangalia uwezekano wa kuona namna gani watashirikiana katika jambo zima la kujenga miundombinu, ili biashara kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo iweze kushamiri? (Makofi)

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba kuna umuhimu mkubwa sana wa kuimarisha barabara sehemu ya pili ya DRC, na kwa hali hiyo tayari saa hizi mazungumzo yameshaanza kati ya DRC na Tanzania na mazungumzo hayo yataendelezwa pia katika Mkutano wa Pamoja wa Ushirikiano (JPC) ambao unatarajiwa kufanyika mwezi Mei na maandalizi wa mkutano huo unategemewa kuanza mwezi wa Aprili. Ahsante sana. (Makofi)