Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 10 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 112 2022-02-14

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI aliuliza: -

Je, lini Serikali inafungua Ubalozi Mdogo katika Jiji la Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa hii ni mara yangu ya kwanza kuzungumza katika Bunge hili, baada ya Mheshimiwa Rais kuniamini kuendelea na nafasi ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, naomba kuchukua fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuniamini. Nami namwahidi kufanya kazi kwa bidii, uaminifu na uadilifu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Cosato Chumi, Mbunge wa Mafinga Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tayari imefungua Konseli Kuu katika Jiji la Lubumbashi, Jimbo la Haut Katanga, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Ofisi za Konseli Kuu hiyo kwa sasa zipo katika Kiwanja namba 1174 Avenue Ruwe, Quartier, Makutano, Jijini Lubumbashi. Ninapenda kulijulisha Bunge lako Tukufu Kuwa Konseli Mkuu tayari amewasili Lubumbashi tarehe 7 Februari, 2022. Aidha watumishi wengine wanaendelea kuripoti katika Kituo hicho kwa awamu kulingana na mahitaji na taratibu za kidiplomasia, ahsante sana. (Makofi)