Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE Aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga Kiwanda cha Parachichi Mkoa wa Iringa hususan Mufindi Kusini?

Supplementary Question 1

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Spika, parachichi ni moja ya mazao saba ya kimkakati ambayo Serikali imeyatangaza, zao la pili kwa Mufindi Kusini ni chai.

Mheshimiwa Spika, naomba kufahamu commitment ya Serikali katika kusaidia wakulima ambao majani yao yanamwagwa wanakosa soko na viwanda havichukui.

Mheshimiwa Spika, swali la pili ziko tetesi kwamba kiwanda hicho kimeuzwa atatusaidia Mheshimiwa Naibu Waziri kama atakuwa na majibu ipi commitment ya Serikali juu ya maslahi ya wafanyakazi kama kweli kiwanda hicho kimeuzwa Mufindi ya Kusini?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile, Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru na nimpongeze Mbunge mwenzangu kutoka Mufindi ambaye anafuatilia sana maendeleo ya wilaya hiyo.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema nia ya Serikali Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wetu mpendwa Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha tunaweka mazingira wezeshi kwa ajili ya maendeleo ya viwanda na hasa tukizingatia kuwa sekta binafsi iwe kiongozi kwa ajili ya kufikia uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Spika, moja ya mikakati ya kukwamua maendeleo katika sekta ya viwanda ni kuhakikisha viwanda vilivyopo vinaendelea, lakini pia kwa ufanisi.

Mheshimiwa Spika, kuhusu viwanda vya parachichi; viko viwanda viwili katika mkoa wa Iringa; Kibidula Avocado Packiging Industry ambayo inafanyakazi vizuri, lakini pia na Kiwanda cha GBRI, Kampuni ya GBRI pale Iringa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Unilever kwa maana ya Kampuni ya Chai, sisi kama Wizara tumeshapata notice ya kuuzwa kwa kampuni hiyo na taarifa hizi ziliifikia Tume ya Ushindani mwaka jana mwezi Desemba kwa maana ya tarehe 17 Desemba, 2021 na hatua zinazochukuliwa kwa kampuni ambayo inauzwa huwa kwanza ni kutangaza notice ya siku 14 kwa wale ambao ni wadau au wanahusika katika mchakato wa kuuza. Kwa hiyo siku zile 14 ziliisha na hakukuwa na mtu yeyote mwenye maoni au malalamiko.

Mheshimiwa Spika, lakini pili sisi kama Serikali kupitia Tume ya Ushindani tunaendelea sasa kufuatilia hatua stahiki za uuzwaji wa kampuni hiyo. Kwa ruhusa yako labda nifafanue kidogo kama utaruhusu kampuni ya Unilever ina kampuni tanzu ya Ekaterra ambayo ndiyo inasimamia sekta ya chai, sasa wanauza kwa Kampuni ya Puchin Bidco ambayo yenyewe itachukua eneo hilo. Kwa hiyo, kwa sasa tumeshaiagiza FCC waendelee kufuatilia na kama kuna watu wenye malalamiko kuhusiana na mauziano haya walete maoni au malalamiko kwenye Tume ya Ushindani.

Mheshimiwa Spika, lakini tatu kuna masuala ya maendeleo ya wafanyakazi nayo yatazingatiwa katika mchakato huo, nakushukuru.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE Aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga Kiwanda cha Parachichi Mkoa wa Iringa hususan Mufindi Kusini?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante; zao la parachichi limekuweko nchini miaka nenda rudi na hata mikoa mingine likiwa ni chakula cha mbwa; hadi majuzi Serikali ilivyoanza kuona kwamba ni zao la kibiashara.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatuambia nini sasa kujenga kiwanda cha kuchakata parachichi katika mkoa wa Kilimanjaro ambapo maparachichi mazuri sana yako kule Rombo, Mwika, Kahe na kwingine ambapo yanatupwa tu hadi leo?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shally Raymond, Mbunge kutoka Kilimanajro kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema mwanzo azma ya Serikali ni kuhakikisha tunaongeza ujenzi wa viwanda kwa kuweka mazingira wezeshi. Kilimanjaro ni moja ya maeneo ambayo yanalima kwa wingi sana parachichi hivyo basi ombi letu ni kuhakikisha na sisi kama wawekezaji tuanze kutumia fursa, kwanza tunaweka miundombinu kupitia SIDO changamoto kubwa tuliyonayo ni collection centers kutunza katika vyumba vya ubaridi matunda yale ili yaweze kuchukuliwa na wenye viwanda. Kwa hiyo kupitia SIDO tutaenda kuhakikisha sasa kunakuwa na ofisi katika ngazi za Halmashauri au Wilaya ili kupunguza upotevu wa mavuno ya matunda yanaposubiriwa kupelekwa kwenye viwanda ambavyo tayari viko nakushukuru sana.