Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 9 Industries and Trade Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji 103 2022-02-11

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DAVID M. KIHENZILE Aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga Kiwanda cha Parachichi Mkoa wa Iringa hususan Mufindi Kusini?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa niaba ya Waziri Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara namba kujibu swali la Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile, Mbunge wa Mufindi Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea na azma ya kuhamasisha ujenzi wa viwanda katika nchi yetu. Moja ya mikakati ambayo Serikali imeweka ni pamoja na kutenga maeneo katika kila Wilaya na kuweka miundombinu wezeshi ili kuvutia uwekezaji wa viwanda kulingana na malighafi zinazopatikana katika eneo husika.

Mheshimiwa Spika, katika Wilaya ya Mufindi, Serikali imetenga maeneo mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa viwanda ikiwemo eneo la Igowole katika Jimbo la Mufindi Kusini. Serikali inaendelea kuhamasisha wawekezaji kujenga viwanda vinavyotumia malighafi zinazopatikana Tanzania ikiwemo zao la parachichi Wilayani Mufindi, nakushukuru.