Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawezesha upatikanaji wa mawasiliano ya simu katika Kata ya Likawage na vijiji vyake vya Likawage, Nainokwe na Liwiti?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Awali ya yote nishukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini pia kwa utekelezaji wa changamoto ya mawasiliano katika Kata ya Likawage.

Mheshimiwa Spika, maswali mawili ya nyongeza; moja, kwa kuwa changamoto ya mawasiliano Kata ya Likawage imedumu kwa muda mrefu na hivyo wana Likawage wanayo furaha sana kwa ambacho Serikali imewafanyia.

Je, Mheshimiwa Waziri atakubaliana kufuatana nami baada ya Bunge hili, ili kwenda kuzindua mnara huo?

Mheshimiwa Spika, lakini la pili, changamoto hiyo iliyopo katika Kata ya Likawage bado pia ipo katika Kata ya Kikole. Je, nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba wanatatua changamoto ya mawasiliano katika Kata ya Kikole? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Mohamed Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kipengele cha kwanza cha swali lake ni ombi la uzinduzi wa minara hiyo. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kazi ya Serikali ni kuhakikisha kwamba inatekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi na sisi tuko tayari kuambatananae na kuhakikisha kwamba, mnara huo unazinduliwa ili wananchi wa eneo husika waendelee kupata huduma ya mawasiliano. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini suala la pili ni kuhusu kata ambayo inachangamoto ya mawasiliano. Ni jukumu la Serikali kwa mujibu wa Ibara ya 61(j) ambapo inatakiwa kuhakikisha kwamba tunafikisha mawasiliano kwa wananchi wote, lakini kabla ya kufanya hivyo lazima tufanye tathmini na kujiridhisha ukubwa wa tatizo na baada ya hapo tutachukua hatua ili kutatua changamoto hiyo. Ahsante. (Makofi)

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawezesha upatikanaji wa mawasiliano ya simu katika Kata ya Likawage na vijiji vyake vya Likawage, Nainokwe na Liwiti?

Supplementary Question 2

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, hali ilivyo katika Jimbo la Kilwa inafanana kabisa na hali ilivyo kwenye Jimbo la Sumve ambapo Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote wakiongozana na Naibu Waziri walikuja kwa ajili ya kuanza ujenzi wa minara katika Kata za Bugando, Mwandu na Lyoma na ujenzi huo leo ni mwaka mzima haujakamilika.

Je, Wizara haioni sasa kuna umuhimu wa kuharakisha ujenzi huu ili watu wa kata hizo waanze kupata mawasiliano kama ilivyo kwenye kata zingine?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kasalali, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, labda kwanza niongee kwamba ujenzi wa minara hii unahitaji vifaa ambayo tunaviingiza kutoka nje ya nchi na kwa sababu ya changamoto ambayo ilikuwepo ya UVIKO-19 uzalishaji wa vifaa hivi katika nchi ambazo tulikuwa tunaagiza ulipungua kwa kiasi kikubwa sana. Kwa hiyo, nina uhakika kabisa, na hii sio changamoto ya Sumve kuna maeneo mengi, na Waheshimiwa Wabunge wengi sana wamelalamika minara katika maeneo yao bado haijasimama kwa muda mrefu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini naomba nitoe taarifa kuanzia sasa mpaka mwezi wa nne tunaenda kuhakikisha minara 288 inawashwa. Hivyo, baada ya kuwasha minara hii baadaye sasa ndio tutajua kwamba changamoto bado imebaki maeneo gani, ili tuweze kuchukua hatua. Nakushukuru sana. (Makofi)