Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 101 2022-02-11

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawezesha upatikanaji wa mawasiliano ya simu katika Kata ya Likawage na vijiji vyake vya Likawage, Nainokwe na Liwiti?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa na kwa unyenyekevu kabisa naomba upokee salamu za pongezi kutoka kwa wananchi wa Jimbo la Bariadi kwa wewe kuchaguliwa kwa kishindo kabisa kuwa Spika wa Bunge letu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kwa niaba ya Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Mohamed Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote tulibaini uwepo wa changamoto ya mawasiliano ya simu katika Kata ya Likawage na vijiji vyake vyote. Hivyo, Serikali ilitangaza kata hii katika zabuni ya awamu ya tano ya mwaka 2021.

Mheshimiwa Spika, kata hiyo ilipata mtoa huduma wa Kampuni ya Tigo iliyokamilisha ujenzi wa minara miwili mnamo mwezi Oktoba, 2021. Ujenzi wa minara hiyo umetatua tatizo la mawasiliano lililokuwepo katika Kata ya Likawage na vijiji vyake. Nakushukuru.