Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha COSTECH inapata fedha za kutosha kwa ajili ya kuwekeza katika STARTUP programu za vijana?

Supplementary Question 1

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante na naishukuru Serikali kwa majibu mazuri na nina maswali mawili madogo ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja, je, ni bunifu ngapi zimeweza kubiasharishwa kutokana na kupata support moja kwa moja na Serikali kupitia COSTECH?

Mheshimiwa Spika, lakini mbili, mwaka jana Serikali mlituahidi ikifika Disemba, 2021 tutaletewa Sera kuhusiana na sayansi, teknolojia na ubunifu. Sasa ningependa kupata commitment ya Serikali kwa sababu mwaka jana halikufanyika; sasa je, Serikali imejipanga vipi kuhakikisha katika mwaka huu Sera ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu mpya inaletwa kwa sababu tuliyonayo ni ya mwaka 1996 na inahusisha sayansi na teknolojia peke yake, haina ubunifu na hivyo haiwezi kuwasaidia vijana katika kujipambanua katika masuala ya ajira ya sayansi, teknolojia na ubunifu? Ahsante. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante na naomba sasa kujibu kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Judith Kapinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, amezuungumzia suala la bunifu ngapi; naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako tukufu kuwa kati ya bunifu 200 zilizoibuliwa kwenye mashindano yetu ya MAKISATU, jumla ya bunifu 26 zinaendelea kuendelezwa na Serikali, ili kufikia dhamira ya kubiasharishwa ili kuleta tija katika jamii. Kwa hiyo, ni bunifu hizo 26. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini eneo la pili amezungumzia suala la sera, naomba tukiri kwamba kulikuwa na ucheleweshaji kidogo wa sera hii yam waka 1996, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge hivi sasa Wizara yangu inaendelea na mapitio ya sera hii na ndani ya mwaka wa fedha 2022/2023 tutaileta sera hiyo hapa Bungeni kwa ajili ya kupitishwa. Nakushukuru sana. (Makofi)