Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 9 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 98 2022-02-11

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha COSTECH inapata fedha za kutosha kwa ajili ya kuwekeza katika STARTUP programu za vijana?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA aliuliza: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Judith Salvio Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua mchango wa STARTUP programu za vijana katika ubunifu na teknolojia kama nyenzo muhimu katika kuongeza tija na ubora katika uzalishaji wa bidhaa, utoaji wa huduma na kuzalisha ajira mpya kwa ajili ya vijana nchini.

Mheshimiwa Spika, ili kuhakikisha Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) inapata fedha za kutosha kwa ajili kuendeleza ubunifu na ubiasharishaji wa teknolojia ikiwemo kupitia STARTUP programu, mwaka 1995 Serikali ilianzisha Mfuko wa Taifa wa Kuendeleza Sayansi na Teknolojia (MTUSATE).

Mheshimiwa Spika, kupitia Mfuko wa MTUSATE, kila mwaka Serikali hutenga fedha kwa ajili ya kuendeleza ubunifu na matokeo ya utafiti unaofanywa nchini kwa lengo la kutatua changamoto zinazoikabili jamii. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 shilingi bilioni 3.5 zimetengwa kupitia mfuko huo. Vilevile kupitia utekelezaji wa Mradi wa Kuendeleza Elimu ya Juu kwa ajili ya Mageuzi ya Kiuchumi COSTECH imetengewa shilingi bilioni 2.13 kwa ajili ya kutekeleza shughuli zake ikiwemo kujenga Mfumo wa Kielektroniki wa Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ambao utawezesha kusajili watafiti, wabunifu, vifaa na miradi ya utafiti na ubunifu pamoja na teknolojia zinazozalishwa hapa nchini na zinazoingia kutoka nje.

Mheshimiwa Spika, Serikali pia inashirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo kuhakikisha kwamba COSTECH inawezesha miundombinu ya ukuzaji ubunifu na ubiasharishaji wa teknolojia ikiwemo uanzishaji wa STARTUP za ubunifu na teknolojia. (Makofi)

Mheshsimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)