Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas Van Zeeland

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne ya ujenzi wa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mzumbe hadi Mgeta?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS V. ZEELAND: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwanza nichukue nafasi hii niipongeze Serikali kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Kwa kuwa changamoto ya barabara iliyopo Mzumbe kwenda Mgeta inafanana kabisa na changamoto ya barabara kutoka Turiani kwenda Mziha mpaka Handeni.

Je, ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami kutoka Turiani kwenda Mziha hadi Handeni?

Swali la pili, kwa kuwa tuna barabara ambayo ndiyo inasafirisha mazao ya wananchi wetu kutoka Kata ya Kibati, Pemba na Wilaya jirani ya Kilindi.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuiongezea bajeti hii barabara ili iweze kutengenezwa kwa kiwango cha kuridhisha na iweze kupitika nyakati zote, lakini pia na kujenga daraja ambalo ni muhimu sana linalounganisha Wilaya ya Kilindi na Wilaya ya Mvomero katika Kata ya Kibati na Kata ya Kinde? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE.ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kwanza nipokee pongeze alizozitoa kwa Serikali kuendelea kufanya kazi katika barabara ambayo ameisema katika swali lake la msingi.

Mheshimiwa Spika, katika barabara aliyoisema ambayo inaanzia Magole – Turiani – Mziha, kipande cha Mziha - Handeni ambacho bado hakijajengwa barabara hii imetengewa bajeti katika mwaka huu wa fedha. Hivyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge awe na subira kadri fedha zitakapopatikana barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami ili kuunganisha Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Tanga - Turiani hadi Handeni.

Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Kibiti ambayo inaenda Kilindi, Tuko kwenye kipindi cha bajeti, ameomba bajeti iongezwe ili tuweze kuijenga kwa kiwango kizuri zaidi. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ombi hilo tumelipokea na tutaangalia namna ya kulifanyia kazi. Ahsante. (Makofi)

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne ya ujenzi wa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mzumbe hadi Mgeta?

Supplementary Question 2

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne pamoja na Rais wa Awamu ya Tano ya ukamilishaji wa ujenzi wa lami kipande cha Mnata -Mugumu mpaka Arusha? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara ya Nata – Mugumu kwenda Arusha ni barabara ambayo inaanzia Makutano- Sanzate – Nata – Mugumu na kuelekea Arusha.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba hadi tunavyoongea mkandarasi yupo site kujenga kilometa 40 kuanzia Sanzate kwenda Nata na baada ya Nata tunafuata Nata kwenda Mugumu. Kwa hiyo, Serikali ina mpango wa kuhakikisha kwamba barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami kadri fedha itakavyoendelea kupatikana. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne ya ujenzi wa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mzumbe hadi Mgeta?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne ambaye aliitoa mwaka 2012 ya kuijenga barabara ya Sangisi - Akeri hadi Ndorombo kwa kiwango cha lami. Ahadi hiyo aliitoa wakati wa mazishi ya aliyekuwa Mbunge wetu Marehemu Jeremiah Sumari? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja na kwa kuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Awamu ya Nne, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba suala hili tutalichukua kwa uzito mkubwa na ikiwezekana baada ya kipindi hiki cha Bunge tukutane tuone kwa nini imechukua muda mrefu ili tuweze kuona namna ya kutimiza ahadi ya Kiongozi wa Taifa. Ahsante. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne ya ujenzi wa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mzumbe hadi Mgeta?

Supplementary Question 4

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa barabara ya Karatu – Mbulu – Hydom – Mkalama – Meatu ni barabara muhimu sana kwa wakazi wa majimbo hayo niliyoyataja.

Je, ni lini Serikali itatekeleza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kama ulivyosema barabara hii ya kutoka Karatu – Mbulu – Hydom - Sibiti kuja Lalagwa – Maswa – Kolandoto ni barabara ambayo inaunganisha mikoa mingi, tayari tupo kwenye manunuzi kipande cha Mbulu – Hydom. Pia Daraja la Sibiti kama nilivyojibu kwenye maswali mengine limeshakamilika na tunategemea kuongeza kilometa 20 pande zote kwenye barabara hiyo. Hali kadhalika, kuanzia Kolandoto tupo kwenye mpango wa kutafuta fedha kuanza ujenzi kutokea Kolandoto kwenda Sibiti. Ahsante. (Makofi)