Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 95 2022-02-11

Name

Jonas Van Zeeland

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne ya ujenzi wa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mzumbe hadi Mgeta?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jonas Van Zeeland, Mbunge wa Mvomero, kama ifuatavyo: -

Barabara ya Mzumbe – Mgeta yenye urefu wa kilometa 26 ni sehemu ya barabara ya Mkoa ya Sangasanga – Langali – Luale hadi Kikeo yenye urefu wa kilometa 59.16 na inahudumiwa na Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).

Mheshimiwa Spika, Ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Mzumbe - Mgeta yenye urefu wa kilometa 26 imeanza kutekelezwa kwa awamu ambapo mwaka 2020 Serikali ilikamilisha ujenzi kwa kiwango cha lami wa kipande cha mita 400 kuanzia Mzumbe na katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali inaendelea na ujenzi wa kipande kingine cha mita 700 kwa shilingi 216,800,000 na kazi ilianza Novemba, 2021 na inatarajiwa kukamilika mwezi Juni 2022. Sehemu iliyobaki itaendelea kujengwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hii ili iendelee kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 kiasi cha shilingi 664,557,000 kimetengwa kwa kazi hiyo. Ahsante.