Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: - Je, Serikali inatumia utaratibu gani wa kugawa miradi ya maendeleo kama shule, barabara na afya inayotokana na Muungano na ina mkakati gani wa kuyapa kipaumbele maeneo ya vijijini ikiwemo Jimbo la Wingwi?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa majibu, lakini pamoja na majibu mazuri nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, pamoja na mambo mengine Wabunge kutoka Zanzibar, pamoja na majukumu mengine tunatakiwa kuwaeleza wananchi wa Zanzibar juu ya umuhimu na faida za Muungano wetu. Kwa kujua hilo, je, Serikali ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar haioni ipo haja ya kuwashirikisha Wabunge kutoka Zanzibar katika uibuaji wa vipaumbele vya miradi inayotokana na fedha za Muungano?

Pili, Mheshimiwa Waziri katika Mkutano wa Nne aliniahidi kwenda Jimboni kwangu kutembelea vijiji vya Mjini Wingwi na Sizini.

Je, ananiahidi ni lini tutakwenda kutekeleza ahadi hiyo?Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omar Issa Kombo, Mbunge wa Wingwi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nikiri wazi kwamba kwa kweli Wabunge kutoka Zanzibar wamekuwa na kipaumbele sana cha kushughulikia changamoto za wananchi wa Zanzibar akiwemo ndugu yangu Omar. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwamba niliahidi kwenda ni kweli, bahati nzuri nilishafika Zanzibar mpaka Jimbo la Nungwi, Jimbo la Amani na maeneo mengine, lakini nikuhakikishie kwamba ahadi yangu ya kufika katika eneo lako la kazi lipo pale pale tutaenda kuchapa kazi ondoa hofu katika hilo.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kushirikisha Wabunge wa Zanzibar naomba niwashukuru, hata hii ajenda ukiangalia fedha za Covid, Wabunge wa Zanzibar mlileta fedha mahsusi hapa wakati mchakato wa barabara ulipokuwa ukifanyika ndiyo maana hata suala zima la fedha za Covid unaona kwamba zaidi ya shilingi bilioni 231 zimeenda upande wa Zanzibar lengo ni kuona kwamba hisia za Wabunge wa Zanzibar zimeonekana kuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba yale Wabunge wanayoyachangia humu katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo lazima iwe shirikishi.

Mheshimiwa Spika, hiyo, hilo jambo ni zuri, tutaendelea kuboresha zaidi jinsi gani Wabunge watashiriki vizuri katika kuibua hoja mbalimbali. (Makofi)