Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 9 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 94 2022-02-11

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza: -

Je, Serikali inatumia utaratibu gani wa kugawa miradi ya maendeleo kama shule, barabara na afya inayotokana na Muungano na ina mkakati gani wa kuyapa kipaumbele maeneo ya vijijini ikiwemo Jimbo la Wingwi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omar Issa Kombo, Mbunge wa Wingwi kama ifuatavyo: -

(a) Serikali zetu zote mbili Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zina dhamira ya dhati ya kuhakikisha kuwa utaratibu wa kugawa miradi ya maendeleo ya Muungano kama shule, barabara na afya unafanyika kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizokubaliwa na pande zote mbili za Muungano. Vipo vigezo vinavyotumika katika kutoa fedha za kugharamia miradi ya Muungano kama vile Sheria ya Mfuko wa Kuchochea Maendeleo ya Jimbo na Sheria nyinginezo zinazotumika kwa pande mbili za Muungano.

(b) Sambamba na hilo, Serikali kupitia misaada ya kibajeti (general budget support) hugawa fedha hizo kwa kigezo kilichokubalika kutumika cha asilimia 4.5 kwa Serikali ya Mapunduzi ya Zanzibar. Aidha, fedha hizo hugawanywa kwenye miradi ya maendeleo kwa kuzingatia vipaumbele vya Serikali ya Mapunduzi ya Zanzibar.

(c) Kwa upande wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini Tanzania (TASAF) Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili uliozinduliwa Februari, 2020, shilingi bilioni 112.9 zimepangwa kutumika Zanzibar ikiwemo katika miradi ya kijamii ambapo kipaumbele ni kwenye maeneo yenye mahitaji zaidi.

(d) Serikali itaendelea kutekeleza vigezo na tatatibu zilizokubaliwa na pande mbili za Muungano pamoja na kuimarisha majadiliano na mashirikiano kwa lengo la kuhakikisha kuwa miradi inayokubaliwa inatatua changamoto zinazowakabili wananchi waliopo maeneo ya vijijini wakiwemo wa Jimbo la Wingwi. Ahsante.