Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ziara kwenye Vituo vya Polisi vya zamani na nyumba za kuishi Askari Unguja na Pemba ili kushuhudia uchakavu uliopo na ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya matengenezo ya Vituo vya Polisi nchini kwa Mwaka 2021/2022?

Supplementary Question 1

MHE. USSI SALUM PONDEZA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza napenda nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini nina swali dogo kabisa la nyongeza la kumuuliza.

Mheshimiwa Spika, tathmini hiyo ambayo imefanywa ya vituo vibovu na nyumba chakavu za askari, lakini katika Jimbo langu la Chumbuni nina vituo viwili ambavyo ni vibovu ambavyo vimefungwa zaidi ya miaka minne. Nataka nimuulize Mheshimiwa Waziri; yuko tayari kuambatana na mimi kwenda katika jimbo langu kwa ajili ya ukarabati wa vituo vyangu ambavyo nimekuwa navidai sasa ni awamu ya pili? Ni lini na yeye yuko tayari nami niko tayari naomba, anisaidie kwa jambo hili. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge wa Chumbuni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, najua katika jimbo lake Kituo cha Kiwanda cha Soda Maruhubi na Kituo cha Chumbuni ndivyo ambavyo vimeathirika sana. Nimwahidi mbele yako kwamba tarehe 22 na 23 mwezi huu wa Februari nitakuwa Zanzibar. Pamoja na mambo mengine nitakayofanya ni kutembelea Vituo vya Chumbuni. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Juma Usonge Hamad

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chaani

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ziara kwenye Vituo vya Polisi vya zamani na nyumba za kuishi Askari Unguja na Pemba ili kushuhudia uchakavu uliopo na ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya matengenezo ya Vituo vya Polisi nchini kwa Mwaka 2021/2022?

Supplementary Question 2

MHE. JUMA USONGE HAMAD: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naitwa Juma Usonge.

Mheshimiwa Spika,Mkoa wa Kaskazini Unguja ni mkoa ambao unaongoza kwa shughuli za kitalii kwa Zanzibar, lakini pia population ya watu ni kubwa sana. Naiomba sana Serikali kupitia Mheshimiwa Waziri; wamejipangaje Wizara hii ili kuhakikisha Mkoa wa Kaskazini Unguja unakuwa na idadi kubwa ya Vituo vya Polisi, ingawa sasa hivi kuna Vituo vitano tu vya Polisi? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juma Usonge Hamad, Mbunge wa Chaani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi, tumefanya tathmini ili tuweze kuona uchakavu wa vituo vilivyopo kwa madhumuni ya kuvifanyia ukarabati. Kwa hiyo baada ya kumaliza zoezi hilo, kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar tutaona maeneo mengine yanayohitaji kuimarishwa ulinzi ili tuweze kuona namna ya kuviongezea nguvu. Ahsante. (Makofi)

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ziara kwenye Vituo vya Polisi vya zamani na nyumba za kuishi Askari Unguja na Pemba ili kushuhudia uchakavu uliopo na ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya matengenezo ya Vituo vya Polisi nchini kwa Mwaka 2021/2022?

Supplementary Question 3

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa matatizo yaliyopo Unguja na Pemba yanafanana sawa na matatizo yaliyopo katika Kituo cha Polisi cha Gonja Maore. Kituo hiki kilijengwa tangu mwaka 1958, kilijengwa kipindi cha Mkoloni. Nyumba zake zote zimechakaa sana, Kituo cha Polisi kimechakaa sana, miundombinu yake hasa maeneo ya toilets hayafai. Je, ni lini sasa Serikali itakwenda kufanya ukarabati katika nyumba hizo? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuena Bushiri, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kweli naomba nitumie nafasi hii kusema kwamba Wizara inatambua uchakavu wa vituo na makazi ya askari katika maeneo mbalimbali nchini. Ndiyo maana tumesema tunafanya tathmini ili kuona kiwango cha uchakavu, tuandae mpango kabambe wa kukarabati vituo hivi. Kwa hiyo, Kituo cha Mheshimiwa Mbunge cha Gonja Maore tutakifuatilia ili kuona katika mwaka ujao nini tunaweza kufanya kukirekebisha kiweze kutoa huduma kwa wananchi wa Gonja. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Ahmed Yahya Abdulwakil

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafanya ziara kwenye Vituo vya Polisi vya zamani na nyumba za kuishi Askari Unguja na Pemba ili kushuhudia uchakavu uliopo na ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya matengenezo ya Vituo vya Polisi nchini kwa Mwaka 2021/2022?

Supplementary Question 4

MHE. AHMED YAHYA ABDULWAKIL: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Naomba nimuulize swali Mheshimiwa Naibu Waziri; kwa kuwa Jimbo la Chukwani wananchi wamejenga kituo kipya cha ghorofa moja na mpaka sasa kimefikia asilimia 85, bado asilimia 15 kimalizike.

Naomba Serikali itoe kauli lini kituo kile kitamalizika na kuanza kutumika na hasa ukitia maanani kwamba lilitokea wimbi kubwa la mauaji katika eneo lile? Ahsante.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Yahya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, napokea ombi au swali lenye mwelekeo wa ombi la Mheshimiwa Yahya, kwamba katika vitu ambavyo tutaviangalia kule ambako wananchi wamejitokeza wakachangia nguvu zao na rasilimali zao nyingine kupitia Mfuko wetu wa tozo tunaweza kuwasaidia ili kukamilisha vituo hivyo. Kwa hiyo katika tathmini itakayofanyika kwa Mheshimiwa Mbunge pia tutapazingatia. Ahsante sana. (Makofi)