Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 8 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 89 2022-02-10

Name

Ussi Salum Pondeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chumbuni

Primary Question

MHE. USSI SALUM PONDEZA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafanya ziara kwenye Vituo vya Polisi vya zamani na nyumba za kuishi Askari Unguja na Pemba ili kushuhudia uchakavu uliopo na ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya matengenezo ya Vituo vya Polisi nchini kwa Mwaka 2021/2022?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ussi Salum Pondeza, Mbunge wa Chumbuni, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilishatembelea na kuona uchakavu wa vituo vya polisi na nyumba za makazi ya askari huko Zanzibar na maeneo mengine ya Tanzania Bara. Zoezi la kufanya tathmini ya uchakavu kujua gharama zinazohitajika ili kufanya ukarabati zinaendelea nchi nzima. Zoezi hili litakapokamilika, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ukarabati kulingana na upatikanaji wa fedha kwa mwaka ujao (2022/2023) kama ilivyofanyika mwaka huu.

Mheshimiwa Spika, katika Bajeti ya Serikali ya mwaka 2021/2022, Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi 2,000,000,000 kwa ajili ya ukarabati wa Vituo vya Polisi na ujenzi wa nyumba za askari. Ahsante sana.