Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mtwara Pachani, Lusewa, Nalasi hadi Tunduru yenye urefu wa kilomita 320 kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pia nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Serikali imesema inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara ile kwa kiwango cha lami na kuna maeneo ambayo hivi sasa magari hayapiti yanakaa siku mbili, tatu kufika mwisho wa safari, kama maeneo ya kutoka Mkandu mpaka Mbesa, eneo la Lusewa mpaka kufika Ligunga na eneo la Majiwe mpaka Milonji ambayo yamekuwa ni maeneo korofi kwa muda mrefu. Je, Serikali haioni sasa haja ya kuweka lami laini katika maeneo hayo ili magari yaweze kupita kwa urahisi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa barabara hii haijawahi kukanyagwa na Naibu Waziri wala Waziri wa Ujenzi, naomba anipe commitment ya yeye na mimi kufuatana kwenda kukagua barabara hiyo ili aone adha wanayoipata wananchi katika maeneo hayo. Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, Mbunge wa Tunduru Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maeneo aliyoyataja ya Lusewa, Mbesa, Malonji nadhani ni jana magari mengi yamekwama. Jana tulitoa maelekezo kwa Mameneja wote wa TARURA Mkoa, naamini watakuwa wananisikia na watakuwa pengine wako site eneo hilo ili waweze kukwamua magari hayo.

Mheshimiwa Spika, hii barabara sasa hivi mwaka huu tumeitengeneza kwa changarawe barabara yote ya kilometa hizi 320. Kwa hiyo nimhakikishie Mbunge kwamba Mhandisi wa Mkoa ninavyosema hivi yuko site kukwamua hayo magari yaliyokwama.

Mheshimiwa Spika, swali la pili; naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na naamini pamoja na Mheshimiwa wa Namtumbo, kwa sababu barabara hii ndiyo barabara muhimu sana kwa watu wa Tunduru na Namtumbo niombe baada ya hapa tupange ziara tutembelee hiyo barabara. Ahsante. (Makofi)

Name

Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mtwara Pachani, Lusewa, Nalasi hadi Tunduru yenye urefu wa kilomita 320 kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Jiji la Arusha linakua kwa kasi sana na kusababisha misongamano mbalimbali, kwa hiyo napenda kufahamu; je, ni lini Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi itaanza rasmi ujenzi wa barabara ya lami ya kutoka pale Kiserian (Moshono) kuunga na bypass na ile ya Ngaramtoni kwenda mpaka Mianzini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mrisho Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali ina mpango wa kujenga hiyo barabara ya kuanzia Moshono kwenda bypass na tayari tumeshaanza, labda ni kuikamilisha tu. Kwa hiyo Serikali bado itaendelea kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, kwa barabara ya pili aliyoitaja ya kuanzia Mianzini kwenda Ngaramtoni yenye urefu wa kilometa 18, ninavyoongea hapa ipo kwenye hatua za manunuzi kuanza kuijenga yote kilometa 18 kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mtwara Pachani, Lusewa, Nalasi hadi Tunduru yenye urefu wa kilomita 320 kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa Serikali iko katika mpango wa kutafuta pesa ya kujenga barabara hiyo ya Mtwara Pachani – Tunduru Mjini.

Je, Serikali haioni haja ya kujenga angalau kilometa tano tu za lami ambapo barabara hiyo inapita Tunduru Mjini Na ofisi zote za Serikali pamoja na taasisi za Kiserikali ziko kwenye barabara hiyo ambapo hakuna lami kabisa na zipo mjini kabisa? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hassan Zidadu Kungu, Mbunge wa Tunduru Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu la msingi, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara nyingi zinazopita katika ofisi zipo ambazo tunazihudumia sisi, lakini pia na TAMISEMI. Tumelichukua hili, tutakutana na wenzetu wa TAMISEMI tuone namna ya kutafuta fedha ili miji hii iweze kupata lami angalau kwa uchache kama miji mingine. Ahsante. (Makofi)

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mtwara Pachani, Lusewa, Nalasi hadi Tunduru yenye urefu wa kilomita 320 kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Barabara ya kutoka Kilindi – Kiteto
– Chemba mpaka Singida ni barabara ya kimkakati ya kuchochea uchumi kwenye mikoa hii minne na wilaya zake. Bajeti hii tunayokwenda kumaliza ilikuwa inaze lakini mpaka sasa michakato yake bado ni mirefu na hatuoni dalili ya kwenda kuanza ujenzi wa barabara hii. Je, ni lini sasa ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami unaanza? Nakushukuru.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kunti Yusuph Majala, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoisema ni sehemu ya barabara inayoanzia Kilindi – Kiberashi – Kiteto hadi Kwamtoro, Singida. Naomba nimhakikishie kwamba kama nilivyosema, barabara hii ndiyo inayopita kwenye Bomba la Mafuta la kutoka Tanzania kwenda Uganda. Kwa hiyo Serikali ya Awamu hii ya Sita imejipanga kuhakikisha kwamba kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha barabara hii inaanza kujengwa. Hivi ninavyoongea barabara hii inaanza kujengwa kwa kiwango cha lami, tuko kwenye hatua za manunuzi kwa barabara hii. Ahsante. (Makofi)