Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 88 2022-02-10

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Mtwara Pachani, Lusewa, Nalasi hadi Tunduru yenye urefu wa kilomita 320 kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Daimu Iddi Mpakate, Mbunge wa Tunduru Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Mtwarapachani – Lusewa – Nalasi – Tunduru yenye urefu wa kilomita 300 ni barabara ya mkoa na inahudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Ruvuma.

Mheshimiwa Spika, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina pamoja na utayarishaji wa nyaraka za zabuni kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami imekamilika mwaka 2020. Baada ya usanifu kukamilika na gharama za ujenzi kujulikana, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, wakati tukisubiri upatikanaji wa fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi, Serikali itaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hiyo ili iendelee kupitika majira yote ya mwaka. Katika Mwaka wa Fedha 2021/2022, jumla ya shilingi milioni 1,960.583 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo mbalimbali na ukarabati wa madaraja kwenye barabara hii. Ahsante.