Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

John Michael Sallu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Kwamsisi mpaka Mkata kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. JOHN M. SALLU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Kule handeni kuna barabara inayotoka Magore - Turiani mpaka Handeni. Barabara hii ina ahadi nyingi za viongozi wa Serikali na vile vile barabara hii inaunganisha Mkoa wa Tanga na Morogoro na ni barabara fupi kwa kuja Jijini Dodoma.

Sasa niulize, ni lini Serikali itamalizia kile kipande cha Turiani - Handeni kwa kiwango cha lami? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa John Marco Sallu, Mbunge wa Handeni Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia barabara zinazopita katika jimbo lake. Kwa swali alilouliza, nataka nimhakikishie kwamba dhamira ya Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan ni kuifungua Tanzania; na kuifungua Tanzania ni kuhakikisha kwamba miundombinu na hasa barabara zinajengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ya Magole - Turiani hadi Handeni ni sehemu ya barabara inayotoka Korongwe - Handeni - Mzia -Turiani - Magole kwenda Kilosa hadi Mikumi. Barabara hii iko kwenye mpango, kwa hiyo, Serikali inatafuta fedha, maana imeshajenga Magole hadi Turiani; sasa hivi inatafuta fedha za kujenga Turiani kwenda Handeni.

MHeshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba iko kwenye mpango wetu na hata kwenye vitabu vya bajeti inaonekana hivyo. Kwa hiyo, avute Subira, barabara itakamilishwa kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Kwamsisi mpaka Mkata kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa nyakati tofauti hapa Bungeni na pia kwenye ziara za viongozi katika Jimbo langu ikiwemo ziara ya Mheshimiwa Waziri Mkuu mwezi Oktoba mwaka 2021, niliiomba Serikali iweze kujenga barabara njia nne kwenda Kipatimu kwa kiwango cha lami ambayo ina urefu wa kilometa 50.

Mheshimiwa Spika, nashukuru Serikali imeanza kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami katika kipande cha kilometa 1.4 katika eneo la mteremko mkali wa Kilimangoge pamoja na eneo la Kijiji cha Ngorongoro:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia eneo lililobaki la kilometa 48.6? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kumba Ndulani, Mbunge wa Kilwa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli katika ziara hiyo nami nilikuwepo na Mheshimiwa Waziri Mkuu kweli aliahidi kwamba barabara hiyo itajengwa. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii tumeichukua na tunaiingiza kwenye mpango kwa ajili ya kujenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, pia napokea pongezi kwamba tayari tumeshaanza kujenga hizo kilometa chache. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba kadiri Serikali itakavyopata fedha, hizi kilomita 48.6 zilizobaki tutajenga barabara kwa kiwango cha lami kuanzia Njia Nne hadi Kilwa Kipatimu.

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Kwamsisi mpaka Mkata kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. PROF. KITILA A. MKUMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Barabara ya Kimara - Mavurunza – Kinyerezi ya kilometa saba maarufu kama Kikwete Highway iliahidiwa na Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete mwaka 2010 na ilikuwepo kwenye Ilani za Uchaguzi tatu; mwaka 2010, 2015 na 2020.

Mheshimiwa Spika, nataka kujua, ni lini ujenzi wa barabara hii utaanza? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Prof. Kitila Mkumbo Mbunge wa Ubungo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba moja ya vipaumbele vya Serikali ni ahadi za viongozi na hasa viongozi wa Kitaifa. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara aliyoitaja ya Kimara kwenda Kinyerezi ambayo iliahidiwa na Mheshimiwa Rais tutaijenga kwa kiwango cha lami kadiri fedha zitakavyoendelea kupatikana. Tunajua baada ya kuwa na Stendi ya Magufuli, hii barabara ni muhimu sana kwa sasa kupunguza msongamano kwenye barabara zetu za Mji wa Dar es Salaam. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Kwamsisi mpaka Mkata kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. TIMETHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Barabara ya Magokweni - Maramba – Daluni – Mashewa Mpaka Korongwe ni barabara muhimu sana kwa uchumi na ulinzi na usalama wa nchi yetu; na kumekuwa na ahadi za viongozi za muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, nataka kujua, ni lini Serikali itatengeneza barabara hii kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mnzava, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge atakuwa shahidi, baada ya Bunge tulilomaliza hii barabara, nimeitembelea kuanzia Mabokweni mpaka Korogwe na hasa kutokana na umuhimu wa hii barabara.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kutafuta fedha. Hata hivyo, kitu tunachokifanya sasa hivi kwa jinsi ilivyopita kwenye miinuko tutaanza kwanza kujenga barabara katika hali zile zenye changamoto ngumu kujenga vipande vifupi vifupi kwa njia ya lami ili njia ipitike kwa muda wote wakati Serikali inatafuta fedha kujenga barabara yote kwa kiwango cha lami. Ahsante.