Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 87 2022-02-10

Name

John Michael Sallu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN M. SALLU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya kutoka Kwamsisi mpaka Mkata kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa John Marko Sallu, Mbunge wa Handeni Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Kwamsisi hadi Mkata yenye urefu wa kilometa 35 ni sehemu ya barabara ya Mkalamo Junction hadi Mkata yenye urefu wa kilometa 73.1. Barabara hii ni ya mkoa na inahudumiwa na Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).

Mheshimiwa Spika, sehemu ya barabara hii kutoka Mkalamo Junction hadi Kwamsisi yenye urefu wa kilometa 38.51 iliingizwa katika mradi wa ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Pangani – Tungamaa – Mkwaja hadi Mkange yenye urefu wa kilometa 95.2. Mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami amepatikana ambaye ni China Railway 15 Group na Mkataba umesainiwa tarehe 6 Septemba, 2021. Gharama za ujenzi ni shilingi bilioni 94.539 na muda wa utekelezaji wa mradi huo ni miezi 48.

Mheshimiwa Spika, sehemu iliyobaki ya Kwamsisi hadi Mkata iliingizwa katika mpango wa RISE (Roads to Inclusion and Socioeconomic Opportunities) ambao inafadhiliwa na Benki ya Dunia. Mradi huu upo katika hatua ya manunuzi ya kumpata Mhandisi Mshauri atakayefanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na kuandaa nyaraka za zabuni kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)