Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje katika kupunguza ama kumaliza kabisa changamoto ya ukosefu wa dawa katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na pia nashukuru kwa majibu sana ya Serikali. Naendelea kuipongeza Serikali kwa juhudi inazofanya kuhakikisha kwamba upatikanaji wa dawa unakuwa ni mzuri. Pia naishukuru Serikali, inajitahidi kuhakikisha kwamba wazee wanapata vitambulisho vya kupata dawa bure na pia wanaendelea kupata vitambulisho vingine. Hata hivyo nina swali la nyongeza kwa Serikali.

Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba wazee wanaendelea kupata stahiki za dawa kwa mwendelezo mzuri bila usumbufu?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa jinsi anavyofuatilia matatizo ya akina mama wa Mkoa wa Pwani kwa ukaribu sana hasa kwenye mahospitali yetu; vile vile kwa jinsi ambavyo anafuatilia watoto wa kike kule mashuleni, niliona procedure yake nzuri sana inayofuatilia kwa karibu sana watoto wakike wa Mkoa wa Pwani.

Mheshimiwa Spika, kwanza niseme kama tulivyosema, mmeona Rais wetu Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan ametoa shilingi bilioni 338.8, shilingi bilioni 495 na umeona shilingi bilioni 18. Kwa kipindi cha miezi tisa tu zimekwenda zaidi ya shilingi bilioni 846. Maana yake ni nini? Shida siyo fedha, ni kujipanga.

Mheshimiwa Spika, kikubwa Waziri wa Afya Mheshimiwa Ummy Mwalimu pamoja na Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Bashungwa wameshatoa maelekezo kwa ma- RMO wote na ma-DMO wote kuhakikisha kila hospitali na kila kituo cha afya na zahanati, wana dirisha la wazee kwenye hospitali zao na kunakuwepo na daktari na mtu maalum wa kuwahudumia wazee. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile kuhakikisha kwamba kunakuwepo na dawa eneo husika na wazee wapate vitambulisho vyao kwa sababu kuna utaratibu wa wazee kupata vitambulisho vyao. Pia tumeshawaelekeza MSD, vituo vyetu vikiomba dawa wapeleke ndani ya siku tatu dawa ziwe zimefika kituoni na kama hawana item hizo, ndani ya masaa 24 wawe wamewaruhusu vituo vinunue dawa kwa sababu imeonekana vituo vinakuwa na fedha za basket fund, na own source lakini wanashindwa kununua dawa kwa sababu hawajapewa ruhusa ya kufanya hivyo kama taratibu zinavyotaka na MSD. Ahsante sana. (Makofi)