Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 8 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 86 2022-02-10

Name

Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE aliuliza: -

Je, Serikali imejipangaje katika kupunguza ama kumaliza kabisa changamoto ya ukosefu wa dawa katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Alice Karungi Kaijage, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imepeleka Bohari ya Dawa (MSD) shilingi bilioni 333.8 kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba ambapo sasa Bohari ya Dawa ipo katika hatua mbalimbali za manunuzi.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kupeleka fedha kwa ajili ya manunuzi, Serikali imetoa shilingi bilioni 18 kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha dawa eneo la Idofi, Mkoani Njombe ambacho kitakuwa na uwezo wa kuzalisha vidonge ndani ya siku mbili vya kutosha nchi nzima kwa miezi mitatu na ujenzi umefikia 70%. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kiwanda cha kuzalisha gloves kilichopo Njombe kimekamilika kwa asilimia 100 na sasa kipo kwenye majaribio; na kikikamilika kitaweza kukidhi mahitaji ya nchi kwa 85%. Aidha, kiwanda cha Keko kimefufuliwa na kinazalisha kwa sasa aina 12 za dawa. Ahsante. (Makofi)