Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: - Je, ni lini Vituo vya Afya vya Nagaga na Mnavira vitakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa sababu mazingira ya ukamilishaji wa vituo hivi umechangiwa kwa namna moja au nyingine kuonekana kwamba kuna maeneo ambayo bado hayajakamilika, kwa mfano Nagaga, Mnavira pamoja na Chiungutwa kuna fedha ambazo hazijatimia pale, kwa sababu bajeti nzima ilikuwa shilingi milioni 500 lakini wamepewa shilingi milioni 400 na hivyo kusababisha baadhi ya majengo kama vile wodi ya akinamama pamoja na majengo ya ultrasound kutokamilika.

Je, ni lini sasa Serikali itakamilisha majengo haya yaliyokosekana? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Issa Ally Mchungahela, Mbunge wa Lulindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa vituo vya afya nchini kote unakwenda kwa awamu. Tunapeleka fedha awamu ya kwanza, tunajenga majengo ya kipaumbele ili kuwezesha vituo kuanza kutoa huduma za msingi, lakini tunatafuta fedha kwa ajili ya awamu ya pili ili kukamilisha majengo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo fedha ambazo zilipelekwa Nagaga na Mnavira zilikamilisha sehemu ya kwanza ya majengo, lakini milioni 100 ambayo inabaki itapelekwa ili kukamilisha wodi ya wanawake pamoja na jengo hilo la ultrasound. Ahsante sana.