Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 83 2022-02-10

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza: -

Je, ni lini Vituo vya Afya vya Nagaga na Mnavira vitakamilika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ally Mchungahela, Mbunge wa Jimbo la Lulindi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2017/2018 Serikali iliipatia Halmashauri ya Masasi shilingi milioni 400 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Nagaga ambapo ujenzi umekamilika na huduma zimeanza kutolewa.

Mheshimiwa Spika, aidha, Halmashauri ya Masasi katika mwaka wa fedha 2021/2022, imetenga shilingi milioni 23 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa nguzo na paa kwenye njia za watembea kwa miguu (walkways).

Mheshimiwa Spika, kati ya mwaka 2009 hadi 2018 kiasi cha Shilingi milioni 110 kilitumika kwa ajili ya ukamilishaji wa boma la OPD la zahanati ya Mnavira. Kati ya fedha hizo shilingi milioni 68 zilitolewa na Serikali na shilingi milioni 42 nguvu za wananchi. Ujenzi wa jengo hilo la Zahanati ya Mnavira umekamilika na huduma zinaendelea kutolewa.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/ 2022, shilingi milioni 500 zimepelekwa Halmashauri ya Masasi kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Chikoropola na Chikundi ambapo ujenzi wa vituo hivi unaendelea. Ahsante.