Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amina Ali Mzee

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza: - Je, Serikali inatumiaje Chuo cha Bahari cha DMI kuendeleza vijana wa Kitanzania ili kukabiliana na changamoto za ajira?

Supplementary Question 1

MHE. AMINA ALI MZEE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza swali moja la nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, natambua wanufaika wakubwa ni vijana Watanzania: Je, Serikali ina mpango gani wa kupanga fedha kwa ajili ya kukiendeleza chuo hiki? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PATROBAS P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, tayari Serikali imeshakuwa na mpango wa kujenga jengo hilo litakalokuwa na urefu wa ghorofa sita na tayari fedha zimeshatengwa kwa ajili ya shughuli hiyo. Kwa hiyo, tunamshukuru sana Mheshimiwa Amina kwa kuwa mfatiliaji.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, tuna habari nyingine njema ambayo Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan ameshatoa zaidi ya shilingi bilioni 54 kwa ajili ya kuwasaidia vijana zaidi ya 150,000 ambao wataenda kupata mafunzo mbalimbali katika vitengo hivyo ikiwemo uchumi wa bahari. Ahsante. (Makofi)

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza: - Je, Serikali inatumiaje Chuo cha Bahari cha DMI kuendeleza vijana wa Kitanzania ili kukabiliana na changamoto za ajira?

Supplementary Question 2

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Chuo hiki cha Bandari ni chuo ambacho kiko kwenye ukanda huu wa Afrika Mashariki, na ni chuo muhimu sana kwa ajili ya mafunzo haya; na kwa sababu vijana wanaokwenda kufundishwa pale wanahitaji kufundishwa kwa vitendo; na kwa sababu chuo hiki kina tatizo la kuwa na meli ya mazoezi. Je, ni lini Serikali sasa itatenga fedha kwa ajili ya kununua meli ya mazoezi kwa ajili ya kuwasaidia vijana kwa ajili ya mafunzo ya vitendo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtaturu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ameuliza ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya mafunzo. Nimhakikishie tu Mheshimiwa kwamba, katika suala hili, pamoja na mambo mengine ya uboreshaji wa chuo hicho, ikiwa ni sambamba na ujenzi unaoendelea, zipo pia fedha ambazo zimetengwa kwa ajili ya vifaa vya kufundishia na kwenye hili suala la meli ni sehemu ya mpango huo. Kwa hiyo kulingana na upatikanaji wa fedha tutalikamilisha hilo na Serikali hii imekuwa ikifanya kazi kwa speed, tutalikamilisha. Ahsante.

Name

Capt. Abbas Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Fuoni

Primary Question

MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza: - Je, Serikali inatumiaje Chuo cha Bahari cha DMI kuendeleza vijana wa Kitanzania ili kukabiliana na changamoto za ajira?

Supplementary Question 3

MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa chuo hiki kinatoa mafunzo ya aina mbili, yaani nadharia pamoja na practical. Sasa swali ni kwamba, je, Serikali inahakikishaje kwamba kwa wale ambao wanamaliza nadharia na wanatakiwa wafanye practical, hiyo practical inapatikana katika meli gani? Nini mchango mchango wa Serikali katika kuhakikisha kwamba upande wa pili wa practical unapatikana? Ahsante sana.

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PATROBAS P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abbas Mwinyi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ameuliza katika eneo la mafunzo, hasa katika practical training. Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Wakala wa TAESA ambaye yuko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, tumekuwa tukitoa mafunzo hayo kwa wahitimu, lakini pia kuna mpango maalum wa chuo chenyewe wa utoaji wa mafunzo ya mabaharia ambao wanahitimiu hapo. Kwa mfano ukiangalia takriban zaidi ya vijana 3,000 waliomaliza katika chuo hicho wamepewa mafunzo. Tunatarajia baada ya marekebisho haya na ukarabati wa chuo pamoja na ongezeko la majengo tayari tutakuwa na uwezo wa kudahili vijana 4,500 hadi 6,500 na hawa wote wanaingia kwenye mpango wa mafunzo. Tumekuwa tukiwapeleka kwenye meli za Wakala binafsi au wawekezaji binafsi pamoja na zile za Serikali.

Mheshimiwa Spika, sasa katika ule mpango wa kupata meli yetu wenyewe kwa ajili ya chou, nao utasaidia katika kufanya practical training ili kuwajengea vijana wetu competence na performance katika kazi hii. Ahsante.