Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 8 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 81 2022-02-10

Name

Amina Ali Mzee

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA ALI MZEE aliuliza: -

Je, Serikali inatumiaje Chuo cha Bahari cha DMI kuendeleza vijana wa Kitanzania ili kukabiliana na changamoto za ajira?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PATROBAS P. KATAMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Ali Mzee, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI) ni Chuo cha Serikali ambacho kimeanzishwa kwa Sheria ya Bunge Na. 22 ya mwaka 1991 Chuo kinatoa elimu na mafunzo katika sekta ya usafiri wa njia ya maji na hivyo kina mchango mkubwa katika kukuza ajira nchini.

Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na changamoto za ajira, Chuo cha DMI kina kitengo maalum cha uwakala wa ajira za mabaharia (DMI Crewing Agency). Kitengo hiki kilianza kazi mwaka 2018. Kina usajili Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) kwa ajili ya kutafuta ajira na mafunzo melini kwa vijana wa Tanzania kwa meli za ndani na nje ya nchi yetu hususan kwenye mashirika mbalimbali ya meli ikiwemo Azam Maritime, Zan Fast Ferry, TPA Kyera, Greece Marine Company na Verba Shipping Company.

Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa kuwawezesha wahitimu wa Chuo cha DMI na mabaharia wa Tanzania kupata ajira katika meli za Kimataifa, Serikali inaendelea na taratibu za kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa Kusimamia masuala ya Bahari duniani (IMO Convention
– Maritime Labour Convention). Kuridhiwa kwa mkataba huu, kutawezesha kutoa mafunzo na ajira kwa mabaharia takriban 150 ambao ni sawa na 25% ya wahitimu kwa mwaka. Ahsante. (Makofi)