Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni lini Ujenzi wa Barabara ya Ifakara – Kihansi – Madeke utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Naomba niulize kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii inaunganisha mikoa ya nyanda za juu kusini; Mkoa wa Morogoro, Mkoa wa Njombe, Mkoa wa Ruvuma, Mkoa wa Mbeya mpaka Rukwa na inatoa alternative route ya barabara ya Iringa - Morogoro yaani kupitia Kitonga. Sasa katika majibu ya Serikali, ameeleza kwa habari ya kipande cha kutoka Ifakara mpaka Kihansi, kuna kipande cha kutoka Kihansi kwenda Masagati - Madeke mpaka Kibena Junction; kipande hiki, zabuni ya kumtafuta Mkandarasi wa kufanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ilitangazwa mwaka wa fedha uliopita, hadi sasa hajapatikana.

Mheshimiwa Spika, swali langu sasa: -

(a) Ni lini sasa Serikali inakwenda kukamilisha kazi hii ya kumpata Mkandarasi huyo?

Mheshimiwa Spika, changamoto kubwa za nchi yetu, Mikoa mingi haijaunganishwa kwa lami; swali langu lingine ni kwamba:-

(b) Ni lini Serikali inakwenda kuunganisha mikoa hii michache ambayo haijaunganishwa kwa lami, ukiwemo Mkoa wa Morogoro?

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kunambi Mbunge wa Mlimba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema, ni lini tunakwenda kuunganisha mikoa yote? Ndiyo kazi inayoendelea. Hata katika jibu la msingi, ndiyo maana hata hii barabara tunaiunganisha kati ya Morogoro na Njombe.

Kwa hiyo, tunaendelea na ni kipaumbele kikubwa sana kwa Serikali kuhakikisha kwamba mikoa hii inaunganishwa kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, Mbunge jitihada unaziona, tayari tunatangaza tender katika kuhakikisha kwamba hizi barabara zinaunganishwa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Mkandarasi upande pili wa kutoka Lupembe - Madeke kuja Taveta, tender inatangazwa tena baada ya kukosa Mhandisi Mshauri. Kwa hiyo, nikuhakikishie kwamba taratibu zinaendelea na Mkandarasi na Mshauri atakapopatikana, ataanza kufanya kazi ya kufanya ufanifu wa barabara hiyo. Ahsante.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni lini Ujenzi wa Barabara ya Ifakara – Kihansi – Madeke utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa barabara ya kutoka Korandoto kuelekea Meatu iko kwenye Ilani: Je, ni lini itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ya Kolandoto ambayo inapita Sibiti kwenda Karatu – Haydom – Mbulu, barabara hii ni ndefu na tuko kwenye mpango wa kuanza kuijenga kipande cha Mbulu kuja Haydom kilomita 50. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge na kipande cha Sibiti tayari daraja limeshajengwa na tutategemea katika bajeti ya mwaka huu na ambayo tunaendelea nayo kuwa na barabara za maingilio zisizopungua kilomita 20 pande zote mbili. Kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari tumeshaanza kutekeleza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni lini Ujenzi wa Barabara ya Ifakara – Kihansi – Madeke utaanza?

Supplementary Question 3

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Naomba kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwanza, naipongeza Serikali kwa kutujengea daraja nzuri linalotuunganisha Wilaya ya Ludewa pamoja na Mkoa wa Ruvuma. Serikali imefanya kazi kubwa sana: -

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara ya Njombe – Ludewa – Manda – Itoni?

Mheshimiwa Spika, barabara hii ikikamilika itakuwa na umuhimu mkubwa sana wa kuunganisha Ludewa pamoja na Ruvuma, lakini vile vile watu wa Ruvuma watapita shortcut baada ya kuzunguka...

SPIKA: Mheshimiwa, swali la nyongeza hilo.

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, vile vile bararabara hii itawezesha mradi wa Liganga na Mchuchuma.

Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Neema Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya Njombe – Ludewa – Manda ni barabara ambayo tayari Serikali imeanza kuijenga. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Tanzania tuna barabara hii tu kilometa 50 ambayo mkandarasi yuko site tunajenga kilometa 50 barabara nzima kwa kiwango cha zege ambayo inakwenda kuunganisha na hilo daraja, hatuna barabara nyingine Tanzania kama hiyo.

Mheshimiwa Spika, lakini pia nataka nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kuanzia junction pale inapotoka barabara kwenda Songea hapa Itoni kwenda Lusitu, hii barabara tayari tunatangaza zabuni kilometa 50 kwenda kuunganisha pale ambapo tumeanza kujenga barabara ya zege ili hatimaye tuweze kukamilisha barabara yote kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Dr. Tulia Ackson

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, ni lini Ujenzi wa Barabara ya Ifakara – Kihansi – Madeke utaanza?

Supplementary Question 4

SPIKA: Ahsante sana. Waheshimiwa Wabunge, tukiwa hapo kwenye Ujenzi na Uchukuzi, nilikuwa nimesema habari ya TARURA, naona Naibu Mawaziri wameshaingia humu ndani, Naibu Waziri anayehusika na TARURA aseme jambo kwa sababu huko tunapigiwa sana simu barabara zimekatika kwenye majimbo.

Sasa kila Mbunge hapa hawezi kupata nafasi ya kueleza, sasa toeni maelekezo ya jumla kwa TARURA nchi nzima ili barabara zinazosimamiwa na TARURA ambazo zimekatika na hazipitiki wao waende wakazitazame ili wananchi waweze kupata huduma ya barabara. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu mwongozo ama maelekezo ambayo Ofisi yako imeyatoa kwetu Ofisi ya Rais, TAMISEMI.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa nimelipata suala hili vizuri, nawaagiza Mameneja wote wa Mikoa wa TARURA pamoja na halmashauri zote nchini kuanzia siku ya kesho waende katika maeneo yote nchi nzima kwenda kufanya tathmini haraka iwezekanavyo na kutupatia Ofisi ya Rais, TAMISEMI kupitia kitengo chetu cha TARURA ili angalau tuweze kutoa fedha katika zile fedha zetu za dharura. Katika yale maeneo ambayo bajeti yake ipo maana yake tutapeleka zile fedha kuhakikisha zinakwenda kufanya hiyo kazi ambayo imekusudiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikuhakikishie tu kabisa hili agizo ambalo tumelitoa litatekelezeka na hiyo taarifa ikishafika tutaileta katika Bunge lako Tukufu kabla ya Bunge hili kwisha. Ahsante sana. (Makofi)