Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 77 2022-02-09

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: -

Je, ni lini Ujenzi wa Barabara ya Ifakara – Kihansi – Madeke utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Godwin Emmanuel Kunambi, Mbunge wa Mlimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Ifakara – Kihansi hadi Madeke yenye kilometa 220.22 ni sehemu ya barabara ya Ifakara – Mlimba – Taweta – Madeke – Lupembe hadi Kibena Mkoa wa Njombe ambayo ni barabara ya mkoa inayounganisha mikoa ya Morogoro na Njombe katika Kijiji cha Madeke.

Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na kuandaa nyaraka za zabuni kwa sehemu ya Ifakara hadi Kihansi yenye urefu wa kilometa 126. Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imeanza maandalizi ya kutangaza zabuni kwa ajili ya kupata Mkandarasi wa ujenzi wa kilometa 50 kati ya Ifakara hadi Mlimba kwa kiwango cha lami ndani ya mwaka wa fedha wa 2021/2022. Aidha, kipande cha barabara kati ya Kihansi na Mlimba chenye urefu wa kilometa 24.26 kimekamilika kujengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, sehemu iliyobaki itaendelea kujengwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha hadi barabara yote ikamilike kwa kiwango cha lami. Pamoja na juhudi hizi, Serikali kwa kutambua umuhimu wa barabara hii, inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali ili kuhakikisha inapitika majira yote ya mwaka ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022, jumla ya shilingi bilioni 2.729 zimetengwa. Ahsante. (Makofi)