Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ramadhan Suleiman Ramadhan

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN aliuliza: - Je, Programu za Mfuko wa Maendeleo ya Vijana (YDF), Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake (WDF), Mfuko wa Taifa wa kuendeleza Wajasiriamali (NEDF) na Mfuko wa kutoa Mikopo kwa Wajasiriamali wadogo (SMF) zimewasaidiaje Vijana, Wanawake na Wajasiriamali wa upande wa Zanzibar katika kujikwamua kiuchumi?

Supplementary Question 1

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri yaliyojibiwa na Mheshimiwa Waziri, lakini nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa ujumla, jibu lake linaonesha kwamba hii mifuko haifanyi kazi Zanzibar na inafanya kazi Tanzania Bara, lakini wapo Watanzania Bara wanaoishi Zanzibar ambao nao walipaswa kunufaika na mifuko hii; ambao hawana sifa ya kunufaika kwenye mifuko kama hii wakiwa Zanzibar. Hawa wananufaikaje? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la rafiki yangu sana Mheshimiwa Ramadhan Suleiman Ramadhan. Ni kwamba kwa wote wanaoishi Bara na kufanya shughuli zao huku Bara, kwa zile fursa zinazohusika na mambo ya Bara zinawagusa huku upande wa bara na wale wote wanaoishi kule Zanzibar na fursa zinazohusika katika mifuko mbalimbali ya Zanzibar, wanapata fursa hiyo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, katika jambo hilo halina shida yoyote, kwa sababu siyo suala la kimuungano. Kwa hiyo, turidhie tu utaratibu wa sasa. Bahati nzuri kule kuna Wizara Maalum inafanya michakato hiyo. Ninaamini, kama kuna maeneo kidogo yanataka uboreshaji, basi inawezekana kwa ushauri mzuri wa upande wa pili, kufanyika uboreshaji wa ziada. Kwa hiyo, hiyo ndiyo hali iliyopo sasa.

Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu hoja yake ni nzuri, inachochea kuona pande zote za Muungano zikiwa na vitu mbalimbali ambavyo vinaweza vikasaidia wananchi katika maeneo haya. Ahsante sana.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN aliuliza: - Je, Programu za Mfuko wa Maendeleo ya Vijana (YDF), Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake (WDF), Mfuko wa Taifa wa kuendeleza Wajasiriamali (NEDF) na Mfuko wa kutoa Mikopo kwa Wajasiriamali wadogo (SMF) zimewasaidiaje Vijana, Wanawake na Wajasiriamali wa upande wa Zanzibar katika kujikwamua kiuchumi?

Supplementary Question 2

MHE. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa biashara ya gesijoto imeshamiri sana duniani na imekuwa inaendelea kwa miaka mingi; na nchi nyingi zimefaidi kwa kuuza gesijoto ambayo inahifadhiwa kwenye misitu; na Tanzania yenyewe hii tunayo misitu mingi iliyohifadhiwa ambayo mojawapo ni ule wa KINAPA na ni mkubwa; naomba nijue mkakati wa Serikali wa kuingia kwenye biashara hii ya carbon trading kwa sababu itatupa fedha kule kwenye vijiji vyetu. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kwa sababu aliyeuliza swali ni mtu mzito katika Kamati ya Mazingira, licha ya kumwomba alete swali hili kama swali la msingi, kwa faida kubwa ni kwamba tuna success story ndani ya nchi yetu katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika. Jambo hili, watu wa Tanganyika zaidi ya 3.2 billion wanakusanya kutokana na Carbonate Hydrates Program.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nadhani jambo hili tutaenda kulichakata vizuri, lakini litakapokuja katika swali la msingi tutalifanyia kazi vizuri kwa heshima ya Mheshimiwa Mbunge. Ahsante.