Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 9 Union Affairs Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 71 2022-02-09

Name

Ramadhan Suleiman Ramadhan

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Primary Question

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN aliuliza: -

Je, Programu za Mfuko wa Maendeleo ya Vijana (YDF), Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake (WDF), Mfuko wa Taifa wa kuendeleza Wajasiriamali (NEDF) na Mfuko wa kutoa Mikopo kwa Wajasiriamali wadogo (SMF) zimewasaidiaje Vijana, Wanawake na Wajasiriamali wa upande wa Zanzibar katika kujikwamua kiuchumi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ramadhan Suleiman Ramadhan, Mbunge wa Chakechake kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Program ya Mifuko yote hiyo iliyotajwa ya kuwaendeleza vijana, wanawake na wajasiriamali, inafanya kazi Tanzania Bara na haitekelezwi upande wa Zanzibar.

Mheshimiwa Spika, mifuko hiyo ilikuwa ni Mfuko wa YDF, WF na NEDF. Namshauri Mheshimiwa Mbunge awasiliane na mamlaka inayohusika na mifuko hii kwa upande wa Zanzibar ambayo ni Ofisi ya Rais Kazi, Uchumi na Uwekezaji ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ili kuona namna ya bora kuwasaidia vijana, wanawake na wajasiriamali wa Zanzibar. Ahsante sana.