Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juliana Didas Masaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. MASABURI aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje katika kudhibiti uchafuzi unaofanyika pembezoni mwa Ziwa Victoria ambao unapunguza samaki kuzaliana?

Supplementary Question 1

MHE. JULIANA D. MASABURI: Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini nina swali moja la nyongeza. Inasemekana samaki na dagaa za Ziwa Victoria zina madini ya zebaki: -

Je, Serikali imefanya tafiti juu ya hili? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, awali ya yote naomba kumpongeza sana dada yangu Mheshimiwa Juliana, kwa kweli yeye ni mwanamazingira mzuri sana. Katika upande huo kuhusu samaki na dagaa wanaopatikana katika Ziwa Victoria kwamba inasemekana wana madini ya zebaki, jambo hilo tuseme kwamba si sawasawa kwa sasa hivi, kwa sababu tunafahamu kwamba tuna-export samaki wengi nje ya nchi na samaki hao wamekuwa wakinufaisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wataalamu wetu hivi sasa wanaendelea kufanya kazi kubwa ya kuhakikisha kwamba katika suala la kanda ya ziwa matumizi mbalimbali ya kemikali yanadhibitiwa, lakini hata hivyo mpaka hivi sasa tafiti mbalimbali zimefanyika na hazijaonyesha kwamba samaki hawa wanaathirika.

Kwa hiyo, kikubwa zaidi tuwaombe wananchi katika maeneo mbalimbali kuendelea kuzingatia masuala mahususi ya kimazingira kwa lengo kubwa la kuendelea kulinda Taifa letu kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Asya Mwadini Mohammed

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. MASABURI aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje katika kudhibiti uchafuzi unaofanyika pembezoni mwa Ziwa Victoria ambao unapunguza samaki kuzaliana?

Supplementary Question 2

MHE. ASYA MWADINI MOHAMMED: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Changamoto hizi za uchafuzi wa kimazingira ambazo zinatokea katika maziwa mbalimbali vile vile hutokea katika fukwe za bahari yetu. Nataka kujua: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kudhibiti uchafuzi huu wa kimazingira kwenye fukwe ukizingatia fukwe hizi tunazihitaji zaidi katika vivutio vyetu vya utalii?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la dada yangu Mheshimiwa Asya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, jambo la kwanza kama Serikali tumeweza kutoa miongozo na hasa kuona jinsi gani tunafanya uratibu wa kufanya recycling process wa taka zote zinazoingizwa baharini. Hata hivyo, mnakumbuka hivi karibuni tuliweza kutoa baada ya kuona pale kuna changamoto kubwa licha ya kuzuia mifuko ya plastic, lakini imeonekana kwamba katika recycles vile vifuniko vya chupa havirejesheki na hivyo mara nyingi sana vimekuwa vikisababisha changamoto kubwa hasa katika samaki baharini.

Mheshimiwa Spika, hivyo, ndiyo maana tumetoa miongozo mbalimbali ya kuhakikisha tunalinda mazingira. Kubwa zaidi tumesisitiza ajenda ya usafi katika maeneo ya miji yote inayozunguka ufukwe wa bahari. Tulitoa maelekezo tulipokuwa pale Kinondoni kwamba maeneo yote yanayozunguka ufukwe wa bahari, Maafisa Mazingira katika maeneo hayo kuhakikisha kwamba ajenda ya usafi kwa wakazi wote inaendelea kwa lengo la kuhakikisha kwamba tunakuwa na mazingira rafiki kwa ajili ya utalii. Ahsante.