Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 7 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 70 2022-02-09

Name

Juliana Didas Masaburi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. MASABURI aliuliza: -

Je, Serikali imejipangaje katika kudhibiti uchafuzi unaofanyika pembezoni mwa Ziwa Victoria ambao unapunguza samaki kuzaliana?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juliana Didas Masaburi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, uchafuzi wa mazingira unaofanyika pembeni mwa Ziwa Victoria unatokana na shughuli za kibinadamu zisizozingatia hifadhi ya mazingira. Shughuli hizo ni pamoja na utiririshaji wa majitaka kutoka katika maeneo ya makazi, utupaji taka ngumu kutoka majumbani na viwandani, kilimo kisicho endelevu kinachosababisha uchafuzi wa maji kutokana na kuongezeka kwa tabaki, matumizi yasiyo sahihi ya viuatilifu na mbolea za viwandani na uchimbaji wa madini usio endelevu.

Mheshimiwa Spika, kutokana na hali hiyo, Serikali imechukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuandaa Kanuni, miongozo na mikakati ya kudhibiti uchafuzi wa mazingira katika maeneo ya maziwa. Aidha, Serikali imeendelea kuhakikisha kuwa tathmini ya athari za kimazingira (TAM) inafanyika kwa miradi ya maendeleo iliyopo inayotarajiwa kufanyika pembezoni mwa Ziwa Victoria ili kuhakikisha udhibiti wa vyanzo vya uchafuzi wa maji ya Ziwa Victoria inayotokana na shughuli za kibinadamu zisizohusisha miradi hiyo unazingatiwa.

Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali imeendelea kuhakikisha kuwa tathmini ya athari za kimazingira (TAM) inafanyika kwa miradi ya maendeleo iliyopo, inayotarajiwa kufanyika pembezoni mwa Ziwa Victoria ili kuhakikisha udhibiti wa vyanzo vya uchafuzi wa maji ya Ziwa Victoria inayotokana na shughuli za kibinadamu zisizohusisha miradi hiyo, inazingatiwa.

Mheshimiwa Spika, vile vile Serikali imepiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastic kwa ajili ya kubebea bidhaa ambayo kwa kiasi kikubwa ilikuwa ikichangia uchafuzi pembeni mwa Ziwa Victoria.