Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMUS H. MAGANGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia Wananchi Pori la Kanegere kwa matumizi ya Wafugaji kwa kuwa Pori hilo limepoteza sifa ya kuwa Hifadhi?

Supplementary Question 1

MHE. NICODEMUS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, Ahsante. Nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini namwomba Waziri apate muda twende tukafanye ziara kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe. Mbogwe ni mji ambao umezingirwa na mapori mengi, hivyo wananchi wa pale wanapata tabu sana jinsi ya kuishi na mapori katikati japokuwa mapori yale hayana sifa ya kuwa na hifadhi. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Waziri siku moja twende tuongozane naye ili kusudi twende tukashauriane vizuri ili wananchi wale waweze kuishi katika hifadhi zile. Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nimepokea ombi hilo na baada ya kikao hiki tutapanga baada ya Bunge tuweke ratiba ya kwenda Mbogwe. Nashukuru sana.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. NICODEMUS H. MAGANGA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia Wananchi Pori la Kanegere kwa matumizi ya Wafugaji kwa kuwa Pori hilo limepoteza sifa ya kuwa Hifadhi?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Matatizo yaliyoko kwenye Pori la Mbogwe ni sawa kabisa na matatizo yaliyoko kwenye Jimbo la Geita Vijijini, Hifadhi ya Rwande, ambayo kimsingi ilishapoteza sifa ya hifadhi.

Sasa ombi langu Mheshimiwa Waziri, atakuwa tayari baada ya vikao hivi kutembelea Jimbo la Geita Vijijini ili aweze kuja kuona lile pori badaye tuwe na utaratibu wa kuwarudishia wananchi waweze kuendelea kulima?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Geita Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, niko tayari kuambatana na Mheshimiwa Musukuma kwenda jimboni kwake na kutembelea pori hilo ili pamoja na Wizara ya Ardhi na wadau wengine tukubaliane namna ya kuli-manage ili wananchi waweze kupata fursa nzuri. Nashukuru sana.