Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 69 2022-02-09

Name

Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. NICODEMUS H. MAGANGA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia Wananchi Pori la Kanegere kwa matumizi ya Wafugaji kwa kuwa Pori hilo limepoteza sifa ya kuwa Hifadhi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Henry Maganga, Nicodemus, Mbunge wa Jimbo la Mbogwe, kama ifatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Pori la Kanegere lina ukubwa wa hekta 725.24 na lipo kwenye Kijiji cha Kanegere ambacho kina eneo lenye ukubwa wa hekta 4,443.35. Kijiji hicho tayari kimeandaa Mpango wa Matumizi ya Ardhi kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi ya Kijiji Na.5 ya mwaka 1999 na Sheria ya Matumizi Ardhi Na.6 ya Mwaka 2007.

Mheshimiwa Spika, Pori la Kanegere linamilikiwa na kijiji na sehemu kubwa ya pori hilo ipo katika safu ya milima. Eneo hilo halifai kwa ajili ya shughuli za ufugaji kwani ni eneo lenye miinuko mikubwa ya milima.

Mheshimiwa Spika, kupitia Mpango wa Matumizi ya Ardhi ulioandaliwa, wananchi wamelitenga eneo hilo kwa ajili ya kuhifadhi na kupunguza mmonyoko wa udongo unaoathiri mazingira ya kijiji kwa ujumla wake. Aidha, kwa upande wa wafugaji mpango huo umetenga eneo la malisho lenye ukubwa wa hekta 405.02 ambalo inashauriwa wafugaji kulitumia kwa ajili ya mifugo yao.

Mheshimiwa Spika, hivyo, natoa wito kwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe kushirikiana na Mamalaka husika ili kukamilisha taratibu za pori hilo kutangazwa rasmi kwenye Gazeti la Serikali kwa manufaa mapana ya Kijiji, Halmashauri na nchi kwa ujumla. Ahsante.