Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: - Je, ni lini Serikali itayachukua Mashamba Pori yasiyoendelezwa kwa Shughuli iliyokusudiwa yakiwepo Mashamba ya Aghakan, Lucy Estate na Gomba Estate na kuyagawa kwa Wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kulikuwa na wananchi wa Kata za Oldonyo Sambu, Mlangarini, Bwanani na Nengung’u ambapo Jeshi limechukua maeneo yao na Serikali ikaahidi kwamba ingewafidia.

Je, ni nini sasa kauli ya Serikali kuchukua maeneo ya mashamba haya ya Tanzania Plantation na Nuru Farm ili wale wananchi waweze kufidiwa kama Serikali ilivyowaahidi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Shamba la Aghakan lililokuwa chini ya Manyara Estate lilikuwa linaajiri zaidi ya watu 2000 kama ajira; na sasa Aghakan imelichukua shamba hilo tangu mwaka 2006 ikisema itajenga Chuo Kikuu: Sasa ni miaka 16 imepita bila kujenga Chuo Kikuu wala kuajiri wananchi hao.

Je, nini kauli ya Serikali kuhusu shamba hilo kukaa miaka 16 bila kuendelezwa? (Makofi)

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu maswali mawili ya nyongeza Mheshimiwa Mbunge wa Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na fidia ya Jeshi, ni kwamba nitawasiliana na wenzetu wa Wizara ya Ulinzi ili waweze kutujulisha vizuri juu yah atua ambazo wameshafikia. Tutakapokuwa tumeshapata taarifa za kina, nitakutana na Mheshimiwa Mbunge ili niweze kumpa mrejesho huo.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na shamba la Aghakan; mwaka 2017, Mheshimiwa Rais aliagiza Wizara nne zikutane ikiwemo Wizara ya Mambo ya Nje, Ardhi, Fedha na Elimu kwa lengo la kuzipatia ufumbuzi changamoto hizo za Taasisi. Hivyo inalazimika kusubiria utekelezaji wa mpango wa uendelezaji uliokusudiwa kutokana na mazungumzo yanayoendelea kati ya taasisi hiyo na Serikali, mazungumzo hayo kwa upande mwingine yanaratibiwa na Wizara ya Fedha.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutakapokuwa tumepata mrejesho au hatua ya mwisho ya mazungumzo hayo, tutamjulisha na hatua stahiki zitafuata. Ahsante. (Makofi)

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: - Je, ni lini Serikali itayachukua Mashamba Pori yasiyoendelezwa kwa Shughuli iliyokusudiwa yakiwepo Mashamba ya Aghakan, Lucy Estate na Gomba Estate na kuyagawa kwa Wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Kutokana na ongezeko kubwa la wananchi ndani ya Jimbo la Momba kwa baadhi ya vitongoji na vijiji: -

Je, ni lini Serikali kwa kupitia Wizara ya Ardhi kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili watakaa kwa pamoja ili kugawa baadhi ya maeneo ambayo ni ya hifadhi ili kuwapatia wananchi wa vitongoji vya Mbao, Ntungwa, Twentela pamoja na Kaonga ili wapate sehemu ya kulima kwa sababu wamekuwa kama wakimbizi?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Condester, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama mnavyojua kwamba nchi yetu inaongozwa na utaratibu wa sheria, ugawaji wa maeneo yote ni jambo linalofuata kisheria. Nami nimwagize tu au nimshauri Mheshimiwa Mbunge kwamba mchakato huu uanze kwao ili watuletee tuweze kupeleka kwa mtu aliyekabidhiwa mamlaka kugawa vipande vya ardhi katika nchi hii, yaani Mheshimiwa Rais, ili sasa utaratibu mwingine uweze kufanyika. Nashukuru. (Makofi)

Name

Priscus Jacob Tarimo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: - Je, ni lini Serikali itayachukua Mashamba Pori yasiyoendelezwa kwa Shughuli iliyokusudiwa yakiwepo Mashamba ya Aghakan, Lucy Estate na Gomba Estate na kuyagawa kwa Wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Naomba kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri swali kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Manispaa ya Moshi imekuwa ikileta orodha ya viwanja ambavyo wamiliki wake hawajaviendeleza kwa muda mrefu:-

Je, ni lini Wizara itaridhia na kufuta viwanja hivyo?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Priscus Tarimo, Mbunge wa Moshi Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyoeleza katika majibu yangu ya msingi, utwaaji wa ardhi yoyote ni jambo la mchakato na utaratibu huo unaanza katika vikao vyenu kule chini katika Halmashauri yenu.

Kwa hiyo, namshauri Mheshimiwa Mbunge, waanzishe mchakato huo, walete katika level ya Wizara, tumpelekee Mheshimiwa Rais kwa hatua nyingine zinazotakiwa kufanyika. Ahsante. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: - Je, ni lini Serikali itayachukua Mashamba Pori yasiyoendelezwa kwa Shughuli iliyokusudiwa yakiwepo Mashamba ya Aghakan, Lucy Estate na Gomba Estate na kuyagawa kwa Wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Changamoto iliyoko Arumeru ya mashamba ambayo hayajaendelezwa iko pia katika Wilaya ya Karatu kwa baadhi ya wamiliki wa mashamba hayo kutokuyaendeleza na hivyo kufanya mapori ambayo yanahifadhi Wanyama ambao wanajeruhi Watoto na wananchi kwa ujumla.

Je, ni lini Wizara itasimamia hili ili mashamba ambayo hayajaendelezwa yaweze kutwaliwa kwa mujibu wa sheria?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, naomba nimjibu Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge wa Viti Maalum, Manyara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa utoaji wa maeneo umeelekezwa kisheria katika Sheria ya Ardhi Na. 4 na Na. 5 na Kanuni zake nyinginezo. Nataka nimwelekeze Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hili kama nilivyoeleza katika majibu mengine ya msingi kwamba hili ni jambo la mchakato, anzisheni mchakato katika maeneo yenu na hatua za kufuatwa juu ya maeneo hayo zitafanyika. Ahsante sana. (Makofi)