Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Makao Makuu ya Tarafa za Basotu, Endasak na Balangdalah kunajengwa Vituo vya Afya?

Supplementary Question 1

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, la kwanza; baada ya ujenzi wa Kituo cha Afya Bassotu, Endasak na Gisambalay kukamilika bado tutakuwa na upungufu wa vituo vya afya 25 kwenye Wilaya ya Hanang’. Je, Serikali iko tayari kutufanyia upendeleo mahususi, ili tupate vituo vya afya viwili kwenye bajeti hii tunayoenda kuianza ya 2022/2023?

Mheshimiwa Spika, lakini la pili; Serikali imetupatia fedha milioni 300 kwa ajili ya kujenga jengo la magonjwa ya dharura kwenye hospitali ya wilaya, lakini wananchi pia, wamehamasishana tumechanga vifaa vinavyokaribia milioni 200. Je, bado tuna upungufu mkubwa wa majengo; Serikali iko tayari kutupatia fedha ili tujenge jengo la wodi kwa ajili ya wanaume? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Samweli Xaday Hhayuma, Mbunge wa Hanang’, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Hhayuma kwa kazi kubwa anayoifanya ya kufuatilia ujenzi wa miundombinu ya huduma za afya kwa ajili ya Jimbo la Hanang’ na nimhakikishie kwamba, Serikali tutaendelea kushirikiana nae kuhakikisha wananchi wa Hanang’ wanapata huduma bora za afya.

Mheshimiwa Spika, upungufu wa vituo vya afya hivi sasa tumeweka mkakati badala ya kujenga kituo cha afya kila kata, tuna kata zaidi ya 3,500 kwa hivyo, kwa sasa tunajenga vituo vya afya vya kimkakati kwenye tarafa, lakini pia kwenye kata zile ambazo zina uhitaji mkubwa kwa maana ya idadi kubwa ya wananchi, umbali mrefu zaidi kutoka kwenye kituo cha karibu, lakini na idadi ya magonjwa.

Mheshimiwa Spiika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutafanya tathmini ya mazingira yale ambayo kimsingi pale Hanang’ tunaweza kujenga vituo vya afya ili tuweze kutafuta fedha kwa ajili ya kujenga vituo hivyo.

Mheshimiwa Spika, pili; ni kweli Serikali yetu imefanya kazi kubwa ya kupeleka fedha ya ujenzi wa miundombinu ya majengo ya dharura, ikiwepo Hanang’ wamepata milioni 300 na kazi ya ujenzi wa wodi na miundombinu mingine tutaendelea kuitekeleza kwa awamu, ili hospitali ile ya Hanang’ iwe na miundombinu yote inayofanana na hospitali ya wilaya. Ahsante. (Makofi)

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Makao Makuu ya Tarafa za Basotu, Endasak na Balangdalah kunajengwa Vituo vya Afya?

Supplementary Question 2

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana nikupongeze kwa kupata nafasi hii. naomba niulize sasa swali dogo la nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, matatizo yaliyopo huko Hanang’ yanafanana kabisa na katika Halmashauri ya Itigi, ambayo ina Tarafa moja. Halmashauri ya Itigi ilikosa pesa za ujenzi vituo vya afya vya tarafa kwa sababu, ni tarafa moja, lakini ina kata 13. Je, sasa Serikali iko tayari kuiangalia kwa jicho la kipekee angalau tukapata kituo kimoja hapa karibuni?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yahaya Massare, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyotangulia kujibu kwenye swali la msingi; kigezo cha ujenzi wa vituo vya afya ni tarafa, lakini pia kata za kimkakati. Kwa hiyo, pamoja na kwamba, Itigi kuna tarafa moja, lakini bado wana sifa ya kupata vituo vya afya kupitia tathmini ya kata za kimkakati.

Kwa hiyo, naomba nilichukue hili na nitawsiliana na Mheshimiwa Yahaya ili tuweze kuona kata zipi za kimkakati tuzipe kipaumbele kwenye awamu zinazofuata za ujenzi wa vituo vya afya. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Makao Makuu ya Tarafa za Basotu, Endasak na Balangdalah kunajengwa Vituo vya Afya?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, katika majibu yake Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba, vituo vya afya vinavyojengwa ni vile vya kimkakati kwa kuangalia na idadi ya watu katika eneo husika. Swali langu; Je, ni lini Serikali itatoa kibali kwa Kituo cha Afya Solwa ambacho kina population kubwa na wananchi wamejitolea kujenga wao wenyewe kile kituo cha afya? Ni lini Serikali itatoa vibali ili kile kituo cha afya cha mkakati kiweze kufanya kazi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christina Mnzava, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa vituo vya afya unajumuisha tathmini za kitaalamu za vigezo ambavyo vinakidhi kujenga kituo cha afya. Na mara wataalamu katika halmashauri husika wakishafanya tathmini na kujiridhisha wananchi wanahamasishwa kuendelea kufanya uchangiaji na ujenzi kwa kutumia nguvu zao wakati Serikali pia inatafuta fedha kwa ajili ya kuwaunga mkono.

Mheshimiwa Spika, kwa hivyo, Kituo cha Afya hiki cha Solwa kama kimeanza ujenzi, bila shaka wataalamu wamefanya tathmini na hakihitaji kibali cha Serikali maana wataalamu wale tayari wameshafanya tathmini na ujenzi umeanza hakuna kibali maalum ambacho kinatolewa, bali ni kuendelea na ujenzi kukamilisha na kusajili kituo ili wananchi waanze kupata huduma.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge aendelee kuwaelimisha Ndugu zangu wananchi wa Solwa kwamba, hatuhitaji kibali, lakini tukamilishe ujenzi na kusajili kwa ajili ya kutoa huduma za afya. Ahsante.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Makao Makuu ya Tarafa za Basotu, Endasak na Balangdalah kunajengwa Vituo vya Afya?

Supplementary Question 4

SPIKA: Ahsante sana. Nilivyosikia neno kibali hapa nikawa natafakari, Mheshimiwa Dkt. Christina Mnzava ni kibali cha kufanya nini?

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, kituo cha afya kilikuwa dispensary, wananchi wakaongeza kuwa kituo cha afya baada ya lile tamko la kika kata kuwa na kituo cha afya. Kwa hiyo, wananchi wamekwishajenga, wodi zimekamilika, OPD imekamilika, kilichobaki ni TAMISEMI kutoa go ahead ili kile kituo kiweze kufanya kazi.

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri nadhani hapo umeelewa hoja yake vizuri. Karibu utoe ufafanuzi.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE):
Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kimsingi alichokuwa anamaanisha Mheshimiwa Dkt. Christina Mnzava ni kukipandisha hadhi kwa maana ya kukisajili sasa kuwa kituo cha afya na sio kibali.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, utaratibu uko wazi, halmashauri wanaandika barua kwenda Wizara ya Afya kupitia Katibu Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, na tunaipandisha hadhi na kuipa namba ya usajili wa kituo cha afya. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mbunge tutashirikiana kupata documents hizo ili tuweze kukisajili kituo hicho kianze kutoa huduma kwa wananchi kwa ngazi ya kituo cha afya. Ahsante. (Makofi)

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Makao Makuu ya Tarafa za Basotu, Endasak na Balangdalah kunajengwa Vituo vya Afya?

Supplementary Question 5

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza: -
Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Naibu Waziri amefika na ametembelea Jimbo la Mbulu Vijijini. Wananchi, wameshajenga vitu vitatu vya afya ambavyo viko hatua mbalimbali; cha Maretadu, Getanyamba na Gembako. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka fedha katika vituo hivi ili kuvimalizia?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Massay, Mbunge w Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kumpongeza Mheshimiwa Mbunge na kuwapongeza wananchi wa Mbulu kwa kazi nzuri wanayoifanya. Na wiki moja iliyopita tukiwa ziara tuliona kazi nzuri sana ya ujenzi wa miundombinu ya huduma za afya.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kazi hii ya ujenzi wa vituo vya afya inafanyika kwa nguvu za wananchi na Serikali kuchangia nguvu za wananchi kupitia aidha, mapato ya ndani ya halmashauri au fedha za Serikali Kuu. Kwa hivyo, naomba nitoe wito kwamba, Halmashauri ya Mbulu Vijijini katika bajeti zao, na bahati nzuri wana zaidi ya bilioni moja na milioni 300 kwa mwaka kwa hiyo, waanze kutenga kwa awamu fedha za kukamilisha baaadhi ya vituo vya afya ambavyo wananchi tayari wamejenga, lakini na sisi Serikali Kuu tutafanya tathmini kuona kiasi cha fedha ambacho kitapatikana kwa ajili ya kuchangia nguvu za wananchi kukamilisha vituo hivi.

Mheshimiwa Spika, kwa hivyo, vituo hivi vitaendelea kukamilishwa kwa awamu. Nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutashirikiana kwa karibu, ahsante. (Makofi)