Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 6 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 43 2022-02-07

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Makao Makuu ya Tarafa za Basotu, Endasak na Balangdalah kunajengwa Vituo vya Afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Samweli Xaday Hhayuma, Mbunge wa Jimbo la Hanang’, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kujenga vituo vya afya katika Tarafa na Kata za kimkakati ambapo, katika mwaka wa fedha 2020/2021 jumla ya shilingi bilioni 58.25 zimepelekwa kujenga vituo vya afya 233 kote nchini.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2021/ 2022 Halmashauri ya Hanang’ ilipokea shilingi milioni 250 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya katika Tarafa ya Simbalay Kata ya Gisambalang na ujenzi unaendelea.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Hanang’ kupitia mapato ya ndani wametenga na kutoa kiasi cha Shilingi milioni 400 kwa ajili ya kuendelea na upanuzi wa Kituo cha Afya Bassotu. Aidha, kiasi cha shilingi milioni 500 kimtengwa katika mwaka 2022/2023 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya kwenye Kata ya Endasak.

Mheshimiwa Spika, Ujenzi wa vituo vya afya katika Halmashauri unajumuisha fedha za mapato ya ndani na maelekezo mahususi yametolewa kwa halmashauri zote nchini kutenga fedha za ujenzi wa vituo ili kuboresha huduma kwa wananchi. Ahsante.