Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza ajira kwa Wahitimu wa Vyuo Vikuu hasa katika Sekta ya Kilimo kwa kuwa mikopo ya Elimu ya Juu imewezesha wanafunzi wengi kuhitimu?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, je, Serikali haioni wakati umefika wa kushirikisha sekta binafsi na taasisi za fedha katika kuwezesha wahitimu wa kilimo kujiajiri kwa uratibu na usimamizi wa Serikali?

Swali la pili; kwa kuwa Benki ya CRDB imeonesha njia ya kushusha riba mpaka asilimia Tisa; je, Serikali haioni kuwa ipo haja sasa kuratibu punguzo hilo la riba, kuweka mpango wa kuwezesha vijana kufaidika na mikopo hiyo kwa ajili ya kilimo?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PASCAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante.

Mheshimiwa Spika, kwanza sekta binafsi na taasisi za fedha ambazo zinaweza zikasaidia vijana pengine kuweza kupata nafasi na kuziratibu kwa ajili ya kuwapa nafasi na fursa, hili tunalichukua kama wazo ambalo tunaweza tukawasiliana na Mheshimiwa Mbunge baadae na kuona namna nzuri ya kuliratibu suala hili ili vijana wetu waweze kupata ajira lakini pia kupata fursa mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, suala la pili ambalo ameliulizia kwa mpango mzuri ambao umeanzishwa na Benki ya CRDB wa kushusha riba kwa asilimia Tisa. Nieleze tu kwamba pia katika ofisi ya Waziri Mkuu tayari tumekwishaanza kuchukua hatua mbalimbali ikiwa kuanzia zile fedha zinazotolewa katika ngazi ya Halmashauri asilimia Nne kwa vijana pia fedha ambazo zimekuwa zikitolewa na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana sambamba na hilo na Mabenki mengine ambayo yamekuwa yakitoa riba mbalimbali tunaendelea kuratibu na tayari mazungumzo yamekwishaanza lakini tutamshirikisha Mbunge ilia one hatua hizo na pengine atakuwa na mawazo ya ziada ambayo yatatusaidia zaidi katika kufikia azma njema ya kuwasaidia vijana wetu. Ahsante. (Makofi)

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza ajira kwa Wahitimu wa Vyuo Vikuu hasa katika Sekta ya Kilimo kwa kuwa mikopo ya Elimu ya Juu imewezesha wanafunzi wengi kuhitimu?

Supplementary Question 2

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, changamoto ya ajira kwa wahitimu wa Vyuo Vikuu wa sekta ya kilimo, zipo pia changamoto zingine kwa sekta mbalimbali. Tumeona kuna changamoto ya wahitimu wa Vyuo Vikuu kwa ajira za Ualimu;

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba hawa Wahitimu wa Vyuo Vikuu wa sekta ya elimu wanapata nafasi za kuajiriwa kwa sababu tumeona wananchi wanachangishwa kwa ajili ya kuweka Walimu katika sehemu mbalimbali, Walimu wa kati wapo wahitimu wengi wamekaa idle? (Makofi)

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri ya awali.

Mheshimiwa Spika, maelezo yanayotoka katika Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Serikali inatambua mahitaji ya Watumishi katika sekta mbalimbali nchini. Naomba niliarifu Bunge lako Tukufu kwamba Mheshimiwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Sita toka alipoingia madarakani aligundua mahitaji ya ajira mpya kwa ajili ya sekta mbalimbali na hivyo mara moja alifanya maamuzi ya kuanza kutoa ajira mpya na mpaka sasa kwa takwimu za mpaka mwezi Januari mwaka 2022 tayari tumekwishaajiri watumishi wapya 11,901 ambao wameshaingia katika sekta mbalimbali mtambuka.

Mheshimiwa Spika, tunajua kwamba ajira hizo 11,901 ni kati ya ajira 40,000 ambazo zilikuwa zimeahidiwa na Mheshimiwa Rais. Naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge tunaendelea kufanya mazungumzo kuangalia Ikama, kuangalia jinsi fedha za ajira ambazo zimeweza kutengwa kwenye Wizara ya Fedha na kama tutakuwa kwenye position nzuri kabla ya kumaliza mwaka huu wa fedha tunataka kuhakikisha kwamba tunaongeza ajira nyingine mpya ili kukidhi mahitaji ya Watumishi katika sekta mbalimbali nchini. (Makofi)

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza ajira kwa Wahitimu wa Vyuo Vikuu hasa katika Sekta ya Kilimo kwa kuwa mikopo ya Elimu ya Juu imewezesha wanafunzi wengi kuhitimu?

Supplementary Question 3

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kuniona. Naomba kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, sababu kubwa ya matokeo mabaya kwa wanafunzi wetu hususan kwa masomo ya hisabati na sayansi yanachangiwa kwa kiasi kikubwa kutokana na uhaba wa Walimu wa Kada hizo. Je, Serikali ina mpango gani wa kuajiri na kuongeza ajira hususan kwa Walimu wanaofundisha masomo ya sayansi na hisabati. Ahsante. (Makofi)

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, tunaendelea kupitia Ikama ya mahitaji ya Walimu na hasa kwenye sekta ya sayansi ili kukidhi mahitaji katika shule zetu.

Mheshimiwa Spika, tumeshafanya mazungumzo na Ofisi ya Rais TAMISEMI ili waweze kutuletea mahitaji na tukishayapata tutapitia tena mahitaji hayo tukilinganisha na bajeti tuliyonayo pia umuhimu wa Walimu hawa wa sayansi.

Mheshimiwa Spika, ninaomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hilo tutalipa kipaumbele, ukizingatia kwamba kwenye kampeni ya Mheshimiwa Rais ya UVIKO tumejenga madarasa mengi, tumejenga vituo vya afya, tumejenga zahanati, kwa hiyo mahitaji haya yote ni muhimu. Na ninaomba niwahakikishie ni dhamira ya Mheshimiwa Rais Mama yetu Samia Suluhu Hassan kuondoa tatizo la Watumishi katika kuhudumia Watanzania na umma mzima wa wananchi wa Tanzania.